…………………………………………………….
Na Mwandishi Wetu
Benki ya Mwalimu (Mwalimu Commercial Bank Plc) inajivunia kutimiza miaka mitano ya mafanikio tangu kuanzia kwake Julai 22, 2016 na kuanza kutoa huduma bora kwa Wateja wake na Jamii kwa ujumla wakiwemo Walimu, Wawekezaji na Wafanyakazi katika Sekta na Taasisi mbalimbali nchini.
Akizungumza mkoani Dar es Salaam katika Makao Makuu ya Benki hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu wa MCB, Richard Makungwa amesema wanajivunia miaka mitano ya mafanikio kutoa huduma bora kwa jamii ya Watanzania hadi kufikia mwaka huu wa 2021 ikiwa pamoja na malengo ya kuboresha mnyororo wa thamani wa Elimu ifikapo 2025 kupitia mkakati wake kupitia ikolojia ya elimu.
0 Comments