Ticker

6/recent/ticker-posts

RC DKT. SENGATI -ASILIMIA 75 YA WAKAZI MIJINI WANAISHI KATIKA MAKAZI HOLELA

Na Anthony Ishengoma-Shinyanga.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati amesema zaidi ya asilimia 75 ya watanzania wanaoishi mjini wanaishi katika makazi holela hali hiyo ikichangiwa na kasi ndogo ya serikali ya kupanga na kupima viwanja katika miji mingi nchini.

Dkt Sengati aliongeza kuwa hali hiyo imepelekea kuwepo kwa makazi yasiyo rasmi katika miji mingi ndiyo maana Serikali kupitia Wizara ya Ardhi na TAMISEMI ilianzisha Programu ya Urasimishaji Nchini ya Mwaka 2013-2023 inayoshirikisha sekta binafsi katika urasimishaji kwa lengo la kuongeza kasi ya upangaji, upimaji na umilikishaji wa ardhi.

Dkt. Sengati alisema hayo jana wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha tathimini ya utekelezaji wa Mpango kazi wa mwaka 2020/2021 kilichokaa jana kupanga malengo ya mwaka, kujadili changamoto za utatuzi wa mogogoro ya ardhi ya wananchi pamoja na kujipanga kukamilisha utekelezaji wa Programu ya Kitaifa ya Urasimishaji Makazi ya 2013-2023.



Aidha Dkt. Sengati aliongeza kuwa lengo la kuongeza kasi ya kupima, kupanga na kurasimisha ardhi kuimarisha usalama wa miliki za ardhi na kuwajengea wananchi uwezo wa kutumia ardhi yao kama mtaji katika maendeleo na uchumi wao na kumwezesha mwananchi kupata hatimiliki kisheria na hivyo kuimarisha usalama wa miliki ya ardhi na kuitumia ardhi hiyo kama mtaji kiuchumi na kimaendeleo.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Bi Jasinta Mboneko aliwataka wataalamu hao wa ardhi kuhakikisha wanamaliza migogoro ya ardhi Mkoani Shinyanga kwa kupima viwanja lakini pia katika upimaji wao wazingatie pia maeneo kwa ajili ya shughuli za kijamii ikiwemo maeneo ya ujenzi wa Shule.

‘’Maeneo yapimwe lakini pia tutenge maeneo ya uwekezaji lakini pia mnapopanga mtenge pia maeneo ya shughuli za kijamii kama maeneo ya Shule ambayo pia ni changamoto kwahiyo tukumbuke maeneo hayo”. Aliongeza Bi Jasinta Mboneko Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga.

Naye Bw. Ezekiel Kitilya Mkurugenzi wa Idara ya Ardhi Mkoa wa Shinyanga alisema kuwa Kikao kazi hicho kinawakutanisha wadau wa Ardhi Mkoa wa Shinyanga ikiwemo Benki ya NMB ambayo inaingia kwa utaratibu mpya utakaohakikisha wananchi wanapata miliki salama ya ardhi na serikali inapata mapato yake.

Bw. Kitilya aliongeza kuwa wadau wa radhi mkoani shinyanga wanakutana pamoja ili kujenga uelewa lakini pia kufanya tathimini ya malengo waliojiwekea kwa mwaka wa fedha ulioisha lakini pia kujipanga upya kwa mwaka mpya wa fedha ikiwemo kujipanga kutekeleza Programu ya Urasimishaji Nchini ya Mwaka 2013-2023.

















Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Bi Jasinta Mboneko akiongea na wadau wa Ardhi wa Mkoa wa Shinyanga waliokaa jana katika ukumbi wa Manispaa ya Shinyanga kupanga malengo ya mwaka na kujadili changamoto za utatuzi wa mogogoro ya ardhi ikiwemo utekelezaji wa Programu ya Kitaifa ya Urasimishaji Makazi ya 2013-2023.


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt Philemon Sengati akifungua Kikao Kazi cha Wadau wa Ardhi Mkoa wa Shinyanga kilichokaa jana kutathimini ya utekelezaji wa Mpango kazi wa mwaka 2020/2021 na kujadili changamoto za utatuzi wa mogogoro ya ardhi ikiwemo utekelezaji wa Programu ya Kitaifa ya Urasimishaji Makazi ya 2013-2023.


Baadhi ya wadau wa Ardhi wa Mkoa wa Shinyanga wakiwa katika kikao kazi cha tathimini ya utekelezaji wa Mpango kazi wa mwaka 2020/2021 kilichokaa jana katika ukumbi wa Manispaa ya Shinyanga kupanga malengo ya mwaka na kujadili changamoto za utatuzi wa mogogoro ya ardhi ikiwemo utekelezaji wa Programu ya Kitaifa ya Urasimishaji Makazi ya 2013-2023.



Baadhi ya wadau wa Ardhi wa Mkoa wa Shinyanga wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Bi. Jasinta Mboneko mara baada ya ufunguzi wa kikao kazi cha tathimini ya utekelezaji wa Mpango kazi wa mwaka 2020/2021 kilichokaa jana katika ukumbi wa Manispaa ya Shinyanga.

Post a Comment

0 Comments