Ticker

6/recent/ticker-posts

JKCI YATOA HUDUMA ZA VIPIMO VYA MAGONJWA YA MOYO KATIKA MKUTANO WA MWAKA WA MADAKTARI


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Tatizo Waane akielezea huduma zinazotolewa na JKCI wakati Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel alipotembelea banda la JKCI wakati wa Mkutano wa mwaka wa madaktari uliofanyika katika Hoteli ya Malaika Jijini Mwanza.

Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Theophilly Mushi akitoa taarifa ya upimaji uliofanyika katika Mkoa wa Geita wakati Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel alipotembelea banda la JKCI wakati wa Mkutano wa mwaka wa madaktari uliofanyika katika Hoteli ya Malaika Jijini Mwanza.


Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Theophilly Mushi akimpima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography – ECHO) mwananchi wa Mkoa wa Mwanza aliyetembelea katika banda la JKCI wakati wa mkutano wa mwaka wa madaktari uliofanyika katika Hoteli ya Malaika Jijini Mwanza

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Tatizo Waane akipokea cheti cha utambuzi wa huduma zinazotolewa na JKCI wakati wa Mkutano wa mwaka wa madaktari uliofanyika katika Hoteli ya Malaika Jijini Mwanza.

Picha na: JKCI

Post a Comment

0 Comments