Ticker

6/recent/ticker-posts

BALOZI MHANDISI AISHA AMOUR AWASILI RASMI WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI


Katibu Mkuu Ujenzi, Balozi Mhandisi Aisha Amour (Kushoto), akipokea zawadi ya maua wakati akiwasili katika ofisi za Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi zilizopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma


Katibu Mkuu Ujenzi, Balozi Mhandisi Aisha Amour akisalimiana na watumishi wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi), mara baada ya kuwasili katika ofisi za wizara hiyo zilizopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dododma. Kulia kwake ni Naibu Katibu Mkuu Ujenzi, Ludovick Nduhiye.


Baadhi ya Viongozi wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi wakiwa wamejipanga kwa ajili ya kumpokea Katibu Mkuu Ujenzi, Balozi Mhandisi Aisha Amour (hayupo pichani), katika ofisi za wizara hiyo, zilizopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma. Kutoka kushoto ni Gabriel Migire - Katibu Mkuu Uchukuzi, Ludovick Nduhiye - Naibu Katibu Mkuu Ujenzi pamoja na Richard Mkumbo - Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango (Sekta Ujenzi).


Katibu Mkuu Ujenzi Balozi Mhandisi Aisha Amour akisaini kitabu cha wageni, mara baada ya kuwasili katika ofisi za Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi zilizopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu Ujenzi, Ludovick Nduhiye (aliesimama), akizungumza jambo wakati wa kikao cha mapokezi na utambulisho baada ya kuwasili kwa Katibu Mkuu Ujenzi, Balozi Mhandisi Aisha Amour (aliyeketi kushoto kwa Naibu Katibu Mkuu Ujenzi), Katika ofisi za Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi zilizopo mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Baadhi ya Wajumbe wa Menejimenti ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, Wakimsikiliza Katibu Mkuu Ujenzi, wakati wa kikao cha Mapokezi na Utambulisho, kilichofanyika leo katika ofisi za Wizara hiyo, zilizopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Post a Comment

0 Comments