Ticker

6/recent/ticker-posts

MATUKIO KATIKA PICHA KWENYE MSIBA WA DKT.MWELECELE NTULI MALECELA


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akitia saini kitabu cha maombolezo katika msiba wa Mtoto wa Mzee John Samuel Malecela Dr.Mwelecele Ntuli Malecela aliyekuwa mfanyakazi wa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam leo.[Picha na Ikulu] 19/02/2022.

Wafanyakazi wa Shirika la Afya Ulimwenguni WHO wakibeba mwili wa marehemu Dr.Mwelecele Ntuli Malecela aliyekuwa mfanyakazi wa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam leo kwa ajili ya kuagwa kabla ya kwenda kuzikwa kijijini kwao Dodoma.[Picha na Ikulu] 19/02/2022.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Majaliwa Kassim Majaliwa mara alipowasili katika msiba wa Mtoto wa Mzee John Samuel Malecela Dr.Mwelecele Ntuli Malecela aliyekuwa mfanyakazi wa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam leo.[Picha na Ikulu] 19/02/2022.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akitoa salamu zake na kutoa pole kwa familia ya Mzee John Samuel Malecela kwa kufiliwa na mtoto wake Dr.Mwelecele Ntuli Malecela aliyekuwa mfanyakazi wa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) hafla iliyofanyika leo katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam leo.[Picha na Ikulu] 19/02/2022.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akitoa salamu zake za mwisho na kuuaga mwili wa marehemu Dr.Mwelecele Ntuli Malecela aliyekuwa mfanyakazi wa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) Mtoto wa Mzee John Samuel malecela leo katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam leo.[Picha na Ikulu] 19/02/2022.

Waziri Mkuu Mstaafu Mzee John Samuel Malecela (katikati) akiwa na familia yake katika msiba wa kumuaga Mtoto wake marehemu Dr.Mwelecele Ntuli Malecela aliyekuwa mfanyakazi wa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) hafla iliyofanyika leo katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam leo.[Picha na Ikulu] 19/02/2022.

Post a Comment

0 Comments