Ticker

6/recent/ticker-posts

TANGA PRESS CLUB WAFANYA BONANZA LA KUHAMASISHA SENSA NA KUTAMBUA JUHUDI ZA RAIS SAMIA SULUHU KATIKA KULETA MAENDELEO NCHINI

MKUU wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba akizungumza wakati wa bonanza hilo kushoto ni Mwenyekiti wa Tanga Press Club Lulu George akifuatiiwa na Bondia Mwakinyo na Afisa Michezo Mkoa wa Tanga Digna Tesha
MKUU wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba akizungumza wakati wa bonanza hilo kushoto ni Mwenyekiti wa Tanga Press Club Lulu George akifuatiiwa na Bondia Mwakinyo na Afisa Michezo Mkoa wa Tanga Digna TeshaMKUU wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba kulia akiwa na Mwenyekiti wa Tanga Press Club Lulu George na Bondia Hassani Mwakinyo wakifuatilia bonanza hilo
MKUU wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandiliwa akizungyumza wakati wa bonanza hilo


Na Mwandishi Wetu,TANGA.

Bonanza la Mama Tumeikita lenye lengo la kuhamasisha zoezi la Sensa ya Watu na Makazi Mkoani Tanga ikiwemo kutambua jitihaza za Rais Samia Suluhu katika maendeleo ya Taifa hapa .

Bonanza hilo ambalo liliandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Tanga *TPC*limefanyika mwishoni mwa wiki Jijini Tanga kwenye viwanja vya Disuza kwa kushirikisha viongozi mbalimbali wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa Bonanza hilo Mkuu wa Mkoa Mgumba alisema aliupongeza uongozi wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Tanga chini ya Mwenyekiti wake Lulu George kwa kuanza na kuratibu bonanza hilo ambalo lilikuwa la aina yake.

Alisema ubunifu ambao umefanywa na uongozi wa klabu hiyo unapaswa kuungwa mkono huku akisema bonanza hilo limefanikiwa sana huku akiwataka viongozi hao kuhakikisha linakuwa endelevu mara kwa mara na kuwahaidi ushirikiano.

“Niwapongeze Tanga Press Club kwa ubunifu huu mkubwa mlioufanya kwa kuhamasisha zoezi la Sensa ya Watu na Makazi na kutambua juhudi za Rais kuwaletea maendeleo wa Tanga limefanikiwa sana nimpongeza Mwenyekiti wa TPC na viongozi wengine kwa kufanikisha bonanza hilo ambalo limewakutanisha pamoja wanajamii wote wa Tanga,viongozi wa mkoa wilaya mpaka vitongoji na waandishi wa habari”Alisema

Alisema kwamba amefurahishwa kwamba na kupendwa na ujumbe uliobebwa kwenye bonanza hilo mama huku akisisitiza umuhimu wa jamii ya wana Tanga kuhakikisha wanaendelea kushiriki zoezi la Sensa ya watu na Makazi ikiwemo kuendelea kuwahabarisha wana Tanga.

Awali akizungumza wakati wa Bonanza hilo Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa aliushukuru uongozi wa Tanga Press Club kuweza kuliandaa bonanza hilo ambalo limewakutanisha wadau mbalimbali kuishiriki katika michezo ambayo ni muhimu kiafya.

Mkuu huyo wa wilaya aliwataka waandishi wa habari mkoani humo waendelee kuboresha mahusiano baina yao kwa wao na taasisi mbalimbali za serikali na kupitia wao wanaweza kuwa na mabonanza mbalimbali huku akiwaomba waone umuhimu wa kufanya

Post a Comment

0 Comments