Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS SAMIA AWEKA SHADA LA MAUA KATIKA ENEO LA KUMBUKUMBU YA MASHUJAA WA NCHI YA MSUMBIJI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitembelea na kuweka shada la Maua katika eneo la Kumbukumbu ya Mashujaa wa nchi ya Msumbiji (Mozambican Heroes’ Square) lililopo Maputo nchini humo tarehe 21 Septemba, 2022. Mhe. Rais Samia aliweka Shada hilo kwa Heshima ya kuwakumbuka Mashujaa wa Msumbiji akiwemo Rais wa Kwanza wa Nchi hiyo Hayati Samora Machel

Viongozi mbalimbali kutoka Tanzania wakiwa katika eneo la Kumbukumbu ya Mashujaa wa nchi ya Msumbiji (Mozambican Heroes’ Square) lililopo Maputo nchini humo tarehe 21 Septemba, 2022.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia vikundi vya ngoma za asili za Msumbiji wakati akitoka kuweka shada la maua kwenye eneo la Kumbukumbu ya Mashujaa wa nchi hiyo (Mozambican Heroes’ Square) lililopo Maputo tarehe 21 Septemba, 2022.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Mji wa Maputo mara baada ya kutembelea Kituo cha uzalishaji wa Nishati ya Umeme nchini Msumbiji tarehe 21 Septemba, 2022.

Post a Comment

0 Comments