Ticker

6/recent/ticker-posts

TANZANIA MWENYEJI WA MASHINDANO YA WANAWAKE MCHEZO WA GOFU


************************

Na Magrethy Katengu

Tanzania imekuwa mwenyeji wa wa Mashindano ya wanawake mchezo wa Gofu Bara la Afrika ulihudhuriwa na nchi mbalimbali 21 ikiwemo Mali,Morocco,Botswana,Afrika kusini,Zambia,Uganda,

Akizungumza Jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Wizara  Sanaa Utamaduni na Michezo Yusufu Omary Wakati wa hafla ya upandishaji bendera za nchi zote zinazoshiriki 21kati ya nchi 54 ambapo amesema Mashindano hayo msimu uliopita yalifanyika nchini Ghana na Tanzania ilishika nafasi ya pili.  

"Niseme kuwa kumekuwa na dhana mchezo huu wa Gofu ni mchezo wa matajiri dhana hii iondolewe kabisa katika Jamii yetu mchezo huu kila mtu ana haki ya kucheza kwani michezo ni sehemu ya burudani na huleta afya"amesema Omari

Aidha Mchezo huu wa Mashindano utafanyika Jijini Dar es salaam ndani ya siku tatu huku Septemba 9 kutakuwa na mashindano mengine na watu wote wapenzi wanakaribishwa kuangalia na kujifunza.

Post a Comment

0 Comments