Ticker

6/recent/ticker-posts

NTDS YAWANOA WATENDAJI NA WENYEVITI WA HALMASHAURI YA KINONDONI



*****************

Na Andrew Chale, Dar es Salaam.

Wizara ya Afya kupitia Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele (NTDS) imetoa mafunzo ya uelewa kwa Watendaji wa Kata na Wenyeviti wa Mitaa ya Halmashauri ya Kinondoni tayari kwa zoezi litakaloanza Novemba 21-25 mwaka huu Jijini Dar es Salaam.

Ambapo Watendaji na Wenyeviti hao, wamepewa mafunzo ya uelewa katika kuelekea kampeni ya ugawaji wa Kingatiba kuthibiti Ugonjwa wa matende na mabusha (Ngirimaji).

Kampeni ya ugawaji wa Kingatiba kuthibiti Ugonjwa wa matende na mabusha (Ngirimaji) inarajiwa kuzinduliwa tarehe 21- 25, Novemba mwaka huu ambapo itafanyika nyumba kwa nyumba katika halmashauri za Temeke, Kinondoni na Ilala Jiji mkoani Dar es Salaam.

Post a Comment

0 Comments