Ticker

6/recent/ticker-posts

TANZANIA MWENYEJI MAONYESHO YA EAST AFRICA PHARMA HEALTHCARE SHOW

Katibu Mtendaji chama cha Wanasayansi wa Maabara(MILSAT) Brian Peter Wiliam akizungumza na waandishi wa habari kuelekea Maonesho Makubwa ya Sekta ya Dawa na Huduma za Afya East Africa Pharma Healthcare yatakayofanyika Desemba 14-16 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Saalam
Msimamizi wa Mradi Thomas James akizungumza na waandishi wa habari kuelekea Maonesho Makubwa ya Sekta ya Dawa na Huduma za Afya East Africa Pharma Healthcare yatakayofanyika Desemba 14-16 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Saalam

Afisa kutoka Chama cha Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (TWCC) Cresensi Mbunda akizungumza na waandishi wa habari kuelekea Maonesho Makubwa ya Sekta ya Dawa na Huduma za Afya East Africa Pharma Healthcare yatakayofanyika Desemba 14-16 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Saalam


*************************

Na Magrethy Katengu

Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Maonyesho makubwa ya sekta ya dawa na huduma za afya East Africa Pharma Healthcare ambayo yatahudhuriwa na wadau na wataalamu wa afya kutoka sehemu mbalimbali Duniani.

Akizungumza na Waandishi wa habari Jijini Dar es salaam Katibu Mtendaji chama cha Wanasayansi wa Maabara (MILSAT) Brian Peter Wiliam amesema maonyesho hayo yanayotarajiwa kufanyika kuanzia Desemba 14-16 kuanzia mwaka katika Ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Saalam ikiwa ni chachu ya kubadilishana uzoefu wa teknolojia ya utabibu mwanadamu na vifaa tiba.

"Tanzania kuwa Mwenyeji wa maonyesho haya itakuwa fursa kubwa kuwakutanisha ya wazalishaji,wauzaji wa dawa,wataalamu wa vifaa tiba kwa ujumla,wafanyabiashara na wasambazaji wa sekta ya uchunguzi wa dawa,Hospitali na watoa ushauri wenye ushawishi mkubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki Nchini ikiwemo nchi ya India iliyo kuwa juu kiteknolojia ya utabibu wa binadamu "amesema Brian.

Hata hivyo Afisa kutoka Chama cha Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (TWCC) Cresensi Mbunda amesema maonyesho hayo yameidhinishwa na Tantrade ikiwa na dhumuni la kutaka Watanzania wapate fursa ya kujifunza, kuimarisha na ushirikianao katika sekta ya Afya baina ya Nchi zitakazo shiriki.

Aidha Msimamizi wa mradi Thomas James amesema makampuni zaidi ya 90 yatashiriki maonyesho hayo na hakutakuwa na kiingilio wananchi wote wanakaribishwa kujifunza na kuona teknolojia ya utabibu katika sekta ya afya kutoka Nchini India.

"Wafanya biashara wa Tanzania watapata fursa ya kukutana na makampuni mengine yanayozalisha vifaa tiba kutoka Nchini India pia Chama Cha wataalamu wa madawa watainyesha fursa za uwekezaji kwa wageni ambazo zinapatikana Nchini "amesema Thomas.

Aidha Wanapenda kushukuru mashirika ya Serikali na binafsi yaliyokubali kushirikiana nasi ikiwemo TPSF, TCCIA, CTI, TANEXA, TMDA, TMSA,MAT,MeLSAT, TANHELSO na TWCC.

Post a Comment

0 Comments