Ticker

6/recent/ticker-posts

JINSI BOLT BUSINESS INAVYOSAIDIA MASHIRIKA NA BIASHARA KATIKA SOKO LA TANZANIA



Dar es Salaam Aprili 2023: Katika kuhakikisha ukuaji wa maendeleo ya uchumi au biashara yoyote inategemea sana ufanisi wa usafiri.

 Hii inatumika kama kiashirio muhimu cha uwezekano wa ukuaji pia ni jukumu muhimu katika maisha yetu ya kila siku. 

Kwa kuwezesha usafirishaji wa watu, bidhaa, huduma na vifaa vingine, usafiri unaruhusu ufikiaji wa huduma na shughuli muhimu kama vile kusafiri kwenda kazini au shuleni, kufanya miamala ya biashara, na kusafiri pia.

Akizungumzia huduma hiyo, Mkurugenzi Mkazi wa Bolt Business nchini Tanzania na Tunisia, Milu Kipimo alisema:

"Huduma ya Bolt Business ilizinduliwa kwa kutoa huduma rahisi kati ya makampuni yote, saizi ya kati hadi makubwa kuweza kusimamia na kulipia huduma ya usafiri ya wafanyakazi wao kupitia malipo ya moja kwa moja kwa mwezi. Tangu kuzinduliwa kwake, Bolt Business imekamilisha malaki ya safari za biashara za mashirika, pamoja na wafanyabiashara wadogo na wa kati kote nchini. Ahadi yetu ya kuboresha safari za kutoka sehemu moja hadi nyingine nchini inaonekana kupitia huduma ya Bolt Business, ambayo inatoa huduma nafuu na rahisi kwa kila usafiri huku ikupunguza wasiwasi wa safari za kikazi kwa makampuni. Lengo letu kuu ni kufanya usafiri kupatikana zaidi na bila usumbufu kwa biashara za ukubwa wowote.”

Aliendelea kusema nchini Tanzania, miundombinu ya usafirishaji bado haijajitoshelezaa katika kukabiliana na ukuaji wa nchi, hivyo kukwamisha upanuzi unaohitajika wa sekta ya biashara na uchumi, na hivyo kuathiri mvuto wa nchi kwa uwekezaji wa moja kwa moja kwa wageni. Miundombinu duni ya barabara, chaguzi chache za usafiri wa umma, na gharama kubwa za usafirishaji kutokana na kuongezeka kwa gharama ya mafuta, ni baadhi ya changamoto zinazokabili soko. Pamoja na mambo haya, pia kuongezeka kwa uendeshaji wa biashara kwa mashirika mengi na vile vile biashara ndogo na za kati. Kwa hivyo, biashara nyingi huishia kuelekeza pesa zao muhimu za usafirishaji na vifaa kwa idara zingine, na hivyo kuzidisha vizuizi vya ukuaji wao katika uchumi ambao tayari unapungua.

Katika muktadha huu ambapo Bolt Business ni toleo la msingi la suluhisho ambalo huruhusu usimamizi wa michakato yote inayohusiana na usafiri na vifaa kwa mashirika, usaidia biashara kwa kutoa jukwaa ambalo hutoa safari za kikazi kwa haraka, zinazofaa, na za bei nafuu.

Bolt Business inatoa uwezo wa kudhibiti na kulipia safari zote za kazi zinazohusiana na biashara ya kampuni husika kutoka kwenye akaunti moja, kuanzia SME hadi mashirika ya kimataifa, huduma za kibunifu na mahususi za Bolt Business huboresha safari za biashara na wateja kwa bonasi ya punguzo la gharama za usafiri. Data inaonyesha kuwa Bolt Business na makampuni yanaweza kutumia unafuu wa hadi 25% kwa safari za kikazi ukilinganishwa na safari za kawaida za teksi.

Huduma ya Bolt Business inatoa faida kadhaa kwa makampuni, ikiwa ni pamoja na:

Kuongezeka kwa tija: Wafanyakazi ambao wanaweza kufikia Bolt Business wanaweza kuomba usafiri kwa urahisi kupitia programu, ambayo huondoa hofu na wasiwasi wa usafiri unaohusiana na mambo ya kazi. Hii inasaidia kubaki kuzingatia kazi zao na hata kufanya kazi wakiwa safarini. Kwa wale wanaochelewa, wanaweza kuomba pikipiki ili kuepuka msongamano wa magari na kufika mahali wanakoenda kwa wakati.

Mipango ya usafiri bila usumbufu kwa wateja, wageni, washirika na wachuuzi: Kwa Ride Booker kampuni zinaweza kufanya mipango ya usafiri kwa wateja wao, wageni, washirika na wachuuzi kwa urahisi. Wanaweza kuchagua aina ya gari inayolingana na bajeti yao na abiria atapokea SMS yenye maelezo ya safari.

Uokoaji wa gharama na uboreshaji wa uhifadhi wa wafanyikazi: Bolt Business imesaidia makampuni kupunguza gharama za usafiri kwa hadi 25%, hata kwa timu kubwa. Zaidi ya hayo, kwa kuwapa wafanyakazi usafiri salama, wa kutegemewa, na wa ufanisi, imethibitisha kuimarisha uhifadhi wa wafanyakazi.

Ufuatiliaji wa safari na usimamizi wa malipo uliorahisishwa: Waajiri wanaweza kufuatilia safari za wafanyakazi kwa urahisi na kudhibiti malipo kupitia “Dashibodi” ya Bolt Business. Hii huondoa usumbufu wa kujaza ripoti za gharama na huruhusu kampuni kudhibiti safari zote za kikazi katika tovuti moja inayofaa.

Utoaji wa huduma za biashara pia umepiga hatua kubwa tangu kuzinduliwa kwake. Bolt Business ilikuwa na rekodi ya ukuaji mkubwa mnamo 2022, na kukua mara nane zaidi ikilinganishwa na mwaka uliopita, na kwa sasa inahudumia takriban kampuni 1000 kote Tanzania. Baadhi ya mashirika hayo ni pamoja na taasisi zinazoongoza za kifedha, vyombo vya habari, viwanda, taasisi za kujitolea, makampuni ya bima, pamoja na NGOs. Ulimwenguni, Bolt Business pia imeendelea kukua kwa kiasi kikubwa na hii imetokana na kuongezeka kwa ushirikiano na wateja waliopo, pamoja na msukumo mkubwa wa kusajili wateja wapya. Kwa hivyo, idadi ya watumiaji mahususi kwenye jukwaa la Bolt Business lilikua kwa asilimia 400% mwaka wa 2022, ikilinganishwa na wakati ule ule mwaka jana, huku idadi ya oda ikiongezeka kwa kiwango sawa.

Bolt inaendelea kuthibitisha msimamo wake kama jukwaa linaloongoza katika tasnia ya usafiri kwa njia ya mtandao nchini Tanzania kupitia huduma zake za kibunifu kwa biashara. Kwa kutoa huduma salama na nafuu yenye utaalamu usio na kifani, kampuni inatanguliza kuridhika kwa wateja kuliko yote mengine.

Kwa habari zaidi kuhusu Bolt Business tembelea tovuti yetu

Post a Comment

0 Comments