Ticker

6/recent/ticker-posts

MIFUMO YA GePG NA NPMIS KUCHOCHEA MAENDELEO

Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo, akisikiliza maelezo kuhusu Mfumo wa Kitaifa wa Usimamizi wa Miradi ya Maendeleo na Programu (NPMIS) kutoka kwa mtaalamu wa Mfumo huo kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Subira Msabaha, wakati wa maadhimisho ya wiki ya Ubunifu yanayofanyika kitaifa Uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Pembejeo (AGITF), Bw. Omar Jumanne Bakari, akisikiliza maelezo kuhusu Mfumo wa GePG kutoka kwa mtaalamu wa Mfumo huo kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Stella Nguma (katikati), wakati wa maadhimisho ya wiki ya Ubunifu yanayofanyika kitaifa Uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Ubunifu na Teknolojia kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia, Dkt. Gerald Kafuku, akisikiliza maelezo kuhusu Mfumo wa GePG kutoka kwa mtaalamu wa Mfumo huo kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Maendaenda, wakati wa maadhimisho ya wiki ya Ubunifu yanayofanyika kitaifa Uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.

Mtaalamu wa Mifumo ya Fedha kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Maendaenda (kushoto) akitoa elimu ya Mfumo wa GePG kwa wanafunzi wa Sekondari Umonga, jijini Dodoma, wakati wa maadhimisho ya wiki ya Ubunifu yanayofanyika kitaifa katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.
Wanafunzi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini Dodoma (IRDP), wakielekezwa namna ya kutumia mfumo wa GePG kulipa ada, wakati wa maadhimisho ya wiki ya Ubunifu yanayofanyika kitaifa katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.





(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WFM, Dodoma)

Post a Comment

0 Comments