Naibu Waziri - Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Patrobas Katambi akifungua Mafunzo ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi kwa Wajumbe wa Jumuiya ya Umoja wa Wabunge Vijana Tanzania yaliyo andaliwa na OSHA Jijini Dodoma.
Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda akitoa wasilisho kwa Wajumbe wa Jumuiya ya Umoja wa Wabunge Vijana Tanzania juu ya majukumu, wajibu na mwenendo wa Taasisi ya OSHA wakati wa Semina ya Mafunzo ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi kwa Wabunge hao iliyofanyika katika Ofisi za OSHA Jijini Dodoma.
Afisa Mafunzo wa OSHA, Bw. Simon Lwaho akiwasilisha mada juu ya namna ya kutambua na kudhibiti aina mbalimbali za vihatarishi vya maeneo ya kazi kwa Wajumbe wa Jumuiya ya Umoja wa Wabunge Vijana Tanzania wakati wa Semina emina ya Mafunzo ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi kwa Wabunge hao.
0 Comments