Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS WA ZANZIBAR ALHAJ DK.HUSSEIN ALI MWINYI AMESHIRIKI MAZIKO YA MJUMBE WA NEC CCM LEO.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi (katikati) pamoja na Viongozi mbali mbali wakiwa katika Sala ya Maiti ya Marehemu Semeni Khamis Vuai Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), iliyoongozwa na Katibu wa Mufti wa Zanzibar Sheikh Khalid Mfaume (mbele) katika Masjid Jamii-Attqwa Dunga na kuzikwa katika Kijiji cha Tunguu Wilaya ya Kati,Mkoa wa Kusini Unguja leo.[Picha na Ikulu] 29/08/2021.

Baadhi ya Viongozi na Waislamu mbali mbali wakimswalia Marehemu Semeni Khamis Vuai Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC),Sala iliyoongozwa na Katibu wa Mufti wa Zanzibar Sheikh Khalid Mfaume (mbele) katika Masjid Jamii-Attqwa Dunga na kuzikwa katika Kijiji cha Tunguu Wilaya ya Kati,Mkoa wa Kusini Unguja leo.[Picha na Ikulu] 29/08/2021.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akifuatana na Mkuu wa Kusini Unguja Mhe.Rashid Hadid Rashid alipowasili katika Masjid Jamii-Attqwa Dunga aliposhiriki katika maziko ya Marehemu Semeni Khamis Vuai Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) aliyefariki jana na kuzikwa leo katika Kijiji cha Tunguu Wilaya ya Kati,Mkoa wa Kusini Unguja.[Picha na Ikulu] 29/08/2021.

Vijana wa Jumuiya ya Vijana (UVCCM) Wilaya ya Kati Unguja wakibeba Mwili Marehemu Semeni Khamis Vuai Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) wakati wa Mazishi yake yaliyofanyika leo katika Kijiji cha Tunguu Wilaya ya Kati,Mkoa wa Kusini Unguja ambapo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi pamoja na Viongozi mbali mbali na Wananchi walihudhuria.[Picha na Ikulu] 29/08/2021.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi (katikati) akitia udongo katika kaburi la Marehemu Semeni Khamis Vuai Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), wakati wa Maziko yaliyofanyika leo katika Kijiji cha Tunguu Wilaya ya Kati,Mkoa wa Kusini Unguja.[Picha na Ikulu] 29/08/2021.

Post a Comment

0 Comments