
Na Richard Mrusha
Msajili wa Vyma vya Siasa nchini ameingilia kati mvutano wa makongamano na mikutano NDANI ya kisiasa kwa kuitisha mazungumzo baina ya vyama vya Siasa, Polisi na Ofisi ya Msajili ili kutafuta suluhu ya mikutano ya NDANI na makongamano.
Msajili wa Vyama vya Siasa, Francis Mutungi ameeleza kushtushwa na kitendo cha polisi kujazana na mabomu katika kila mkutano wa chama cha siasa nchini jambo linaloleta taswira hasi kuwa hali ya kisiasa nchini si shwari wakati si kweli.
Tunafanya jitihada kuondosha mvutano kati ya Polisi na Vyama vya Siasa, niliwasiliana na IGP na tukakubaliana tuwaite Wadau, katika kikao hicho. Tutawaita Polisi wakiongozwa na IGP, Viongozi wa Vyama pamoja na Ofisi ya Msajili.
Siasa Nchi yetu haijafika hatu ahiyo ya taharuki ambazo hazina mbele wala nyuma, ni suala tu la kuwekana sawa, tunataka kuondoa hicho kitu ambacho Polisi wanaona Wanasiasa wanaona Polisi wanakosea hapa.
Niwakumbushe tu licha ya Mkutano unaokuja kati ya Polisi, Vyama na Msajili, bado kuna fursa nyingine ambayo Wanasiasa kama kuna changamoto nyingine huo ni muda mwafaka wa kuzitoa.
MAAMUZI YA MSAJILI NI YAKUPONGEZWA.
Uamuazi wa Msajili wa Vyama vya Siasa kuitisha Kikao kati ya Mkuu wa Jeshi la Polisi na Vyama vya siasa ni Uamuzi sahihi. Polisi wamekuwa wakidaiwa na vyama vya siasa kuwa wanavunja Sheria na kuzuia Vyama kufanya kazi zao za kisheria. Wakati huo huo Polisi nao wamekuwa wakidai vyama vya siasa vinavunja Sheria za Jeshi la Polisi hivyo
Mkutano huo ni muhimu kwa Afya ya demokrasia yetu na usichelewe Vyama vifanye kazi zao za kisiasa kwa Uhuru na wakati huo huo Jeshi la Polisi litekeleze majukumu yake kwa mujibu wa sheria.
Kutokana na hatua hii ya msajili kwa busara ya kawaida tu vyama vya siasa wangesitisha mikutano yao na makongamano ili kupisha mkutano huu muhimu kwajili ya Amani na demokrasia yetu.
0 Comments