Ticker

6/recent/ticker-posts

MATUKIO KATIKA PICHA: KONGAMANO LA WAJASIRIAMALI KATIKA MAONESHO YA NGUVU KAZI / JUA KALI, JIJINI MWANZA

Mkuu wa Kitengo cha KAIZEN kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara Bi. Jane Lyatuu akitoa mada wakati wa kongamano la Wajasiriamali katika Maonesho ya 21 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati wa Afrika Mashariki (Nguvu Kazi / Jua Kali) yanayofanyika Rock City Mall, Jijini Mwanza.


Sehemu ya wajasiriamali wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwakilishwa katika kongamano katika Maonesho ya 21 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati wa Afrika Mashariki (Nguvu Kazi / Jua Kali) yanayofanyika Rock City Mall, Jijini Mwanza.


Mkurugenzi wa Forodha na Biashara kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Bw. Kenneth Bagamuhunda akitoa mada kuhusu Biashara kwenye maeneo ya Mipaka katika kongamano hilo.


Mwenyekiti wa Wajasiriamali Jumuiya ya Afrika Mashariki Bw. Josephat Rweyemamu akieleza jambo wakati wa kongamano hilo la wajasiriamali lililofanyika Rock City Mall, Jijini Mwanza.

Sehemu ya Maafisa kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa kwenye kongamano hilo la Wajasiriamali katika Maonesho ya 21 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati wa Afrika Mashariki (Nguvu Kazi / Jua Kali) yanayofanyika Rock City Mall, Jijini Mwanza.

PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU

Post a Comment

0 Comments