Ticker

6/recent/ticker-posts

MWAKA MPYA WA 2022 WATENDAJI WA NIC MNATAKIWA KUWA NA MTAZAMO MPYA-DORIYE

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Bw.Elirehema Doriye akizungumza na watumishi wa Shirika hilo leo wakati wa mkutano wa kufunga mwaka uliofanyika katika ukumbi wa NIC Jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Masoko na Huduma kwa Wateja (NIC), Bw.Yessaya Mwakifulefule akizungumza wakati wa mkutano wa kufunga mwaka uliofanyika katika ukumbi wa NIC Jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Bw.Elirehema Doriye akigawa cakula cha mchana kwa watumishi wa Shirika hilo leo wakati wa mkutano wa kufunga mwaka uliofanyika katika ukumbi wa NIC Jijini Dar es Salaam. Watumishi wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo wakati wa mkutano wa kufunga mwaka uliofanyika katika ukumbi wa NIC Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

**************************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Watumishi wa Shirika la Bima la Taifa (NIC ) wametakiwa kujiandaa kwenda na mabadiliko yatayojitokeza katika soko kwa mwaka mpya wa 2022 ili kuweza kuinua na kuendelea kuwa juu Shirika hilo.

Wito huo umetolewa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo Bw.Elirehema Doriye wakati wa mkutano wa kufunga mwaka uliofanyika katika ukumbi wa NIC Jijini Dar es Salaam.

Amesema mwaka mpya wa 2022 watendaji wa NIC Wanatakiwa kuwa na mtazamo mpya,utendaji wenye ubunifu na uadilifu wa hali ya juu ili kuwahudumia watanzania kwa kiwango chenye ubora uliotukuka.

" Kuanzia mwaka 2002 NIC imekuwa ikikuwa katika utoaji huduma zake mpaka hivi leo lakini mwaka ujao unapaswa kuwa bora zaidi kushinda miaka yote ilyopita kwa kuongeza ufanisi katika kazi ikiwa ni pamoja na juhudi binafsi" Amesema Bw.Doriye.

Amesema jambo la kumshukuru Mungu kumaliza mwaka wakiwa salama na wamoja katika utendaji kazi ambao umekuwa chachu katika ujenzi wa taifa.

Post a Comment

0 Comments