Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS MHE.DKT.HUSSEIN MWINYI AZINDUA MATEMBEZI YA UVCCM KUSHEREHEKEA MIAKA 58 YA MAPINDUZI MATUKUFU YA ZANZIBAR VIWANJA VYA KONDE PEMBA

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi ambae ni Mlezi wa Matembezi hayo ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) kuadhimisha Miaka 58 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,baada ya kuyazindua leo 3-1-2022, katika viwanja vya mpira Konde Mkoa wa Kaskazini Pemba.(Picha na Ikulu)

MLEZI wa Matembezi ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi akizungumza na Vijana wa Mikoa ya Tanzania Bara na Zanzibar wanaoshiriki Matembezi ya kusherehekea Miaka 58 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, yaliyozinduliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi katika viwanja vya Konde Mkoa wa Kaskazini Pemba leo 3-1-2022.(Picha na Ikulu)

NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt.Abdalla Juma Mabodi akizungumza na Vijana wa UVCCM kabla ya kumkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, kuzungumza na Vijana washiriki katika matembezi ya kusherehekea Miaka 58 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, yaliozinduliwa katika viwanja vya Konde Mkoa wa Kaskazini Pemba.(Picha na Ikulu)

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikmkabidhi picha ya Kiongozi Muasisi wa Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume,Mshiriki wa Matembezi ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) kusherehekea Miaka 58 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.Mhe.Asya Sharif, baada ya kuyazindua katika viwanja vya Konde Mkoa wa Kaskazini Pemba leo 3-1-2022, kuaza matembezi hayo Kisiwani Pemba.(Picha na Ikulu)

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikmkabidhi Bendera ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mshiriki wa Matembezi ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) kusherehekea Miaka 58 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.Ndg Abdalla Koti, baada ya kuyazindua katika viwanja vya Konde Mkoa wa Kaskazini Pemba leo 3-1-2022, kuaza matembezi hayo Kisiwani Pemba.(Picha na Ikulu)

VIJANA wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wakiwa wamebeba picha za Viongozi wakishiriki katika matembezi ya kuadhimisha sherehe za Miaka 58 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, baada ya kuzinduliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi.(hayupo pichani) katika viwanja vya Konde Mkoa wa Kaskazini Pemba leo.3-1-2022.(Picha na Ikulu)

VIJANA wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wakishangilia wakati wa Uzinduzi wa Matembezi ya kusherehekea Miaka 58 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, katika viwanja vya Konde wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akihutubia na kuyazindua kuaza matembezi hayo katika Mikoa ya Pemba leo 3-1-2022, katika viwanja vya Konde Pemba.(Picha na Ikulu)

Post a Comment

0 Comments