Ticker

6/recent/ticker-posts

SERIKALI YASIKIA KILIO CHA MBUNGE MPINA UKOSEFU WA HUDUMA KWENYE ZAHANATI JIMBO LA KISESA

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Innocent Bashungwa.
**********************

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Innocent Bashungwa amesikia kilio cha Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina aliyehoji sababu ya Serikali kutozifungua Zahanati 10 zilizojengwa na kukamilika kwa miaka mingi sasa huku wananchi wa vijiji hivyo wakilazimika kutembea umbali mrefu kutafuta huduma.

Akichangia bajeti ya Wizara ya Afya bungeni Dodoma Mei,2022, Mpina alisema upungufu wa watumishi wa kada ya Afya ngazi ya Zahanati ni tatizo ambalo halijapata suluhu kwa muda mrefu na wananchi wakiendelea kukosa huduma hitajika katika vijiji vingi vya Jimbo la Kisesa.

Mpina alisema Serikali ilipaswa kuweka utaratibu mzuri wa ajira na kutumia njia mbadala ya kuingia 4 mkataba na vijana waliohitimu mafunzo mbalimbali ya Afya ambao hawaja ajiriwa ili kusaidia utoaji wa huduma kwa wananchi.

“Mheshimiwa Spika, Kwenye Jimbo langu la Kisesa nina Zahanati 10 zilizokamilika muda mrefu lakini huduma hazitolewi, Mfano Zahanati ya Kijiji cha Semu, Mwandu Kisesa, Makomangwa, Mwageni, Mwagayi, Isangijo, Ikigijo, Mwakisandu, Malwilo na Tindabuligi, lakini pia tuna maboma ya muda mrefu 10 ya Kijiji cha Inonelwa, Mwamhongo, Nzanza, Matale, Masanga, Mwakipugila, Ntobo, Ng’hanga, Mwakasumbi na Lubiga” alisema Mpina.

Hata hivyo kwa mujibu wa orodha ya majina ya watumishi wapya wa sekta ya Afya iliyotangazwa na Waziri Bashungwa Juni 26, 2022 kwa Jimbo la Kisesa zitafunguliwa Zanahati 6 kati ya 10 zilizokamilika ujenzi wake.

Waziri Bashungwa amezitaja Zahanati hizo mpya zilitakazofunguliwa rasmi kwa Jimbo la Kisesa na idadi ya watumishi wapya kwenye mabano kuwa ni Zahanati ya Kijiji cha Isangijo Kata ya Lubiga (3), Zahanati ya Kijiji cha Makomangwa Kata ya Mwandoya (3), Zahanati ya Kijiji cha Mwagayi Kata ya Itinje (3).

Pia Waziri Bashungwa amezitaja zahanati nyingine zitakazofunguliwa Jimbo la Kisesa kuwa ni Zahanati ya Mwageni Kata ya Isengwa (3), Zahanati ya Kijiji cha Mwasungura Mwageni B (2), Zahanati ya Kijiji cha Malwilo Mnadani Kata ya Tindabuligi (3), Zahanati ya Mwandu Kisesa Kata ya Kisesa (3).

Waziri Bashungwa amewataja watumishi hao na majina ya vituo vyao kwenye mabano kuwa kuwa ni Teodora Kalistus Chodota Muuguzi Daraja la II, Ayubu Gladwell Mwaibosi Muuguzi Daraja la II na Ramadhani Shabani Mrutu, Tabibu Daraja la II (Co) (Zahanati ya Isangijo).

Wengine ni Joseph Rashid Ghake, Muuguzi Daraja la II, Edomu Anania Mwakingwe, Muuguzi Daraja La II, Frank John Mandala Tabibu Daraja la II (Zahanati ya Makomangwa).

Bashungwa amewataja wengine kuwa ni Nuru Daud Mwala , Muuguzi Daraja la II na Ernest Joseph Kachwele, Muuguzi Daraja la II (Zahanati ya Malwilo). Wengine ni Samwel Gelewa Simon, Muuguzi Daraja la II, Maryam Baraka Omar Female, Tabibu Daraja la II (CO) na Yohana Magori Magori, Muuguzi Daraja la II (Zahanati ya Mwagayi).

Wengine ni Azizi Poul Mgoboleni, Tabibu Daraja La II (Co), Johnson Joseph Kayombo, Muuguzi Daraja la II na Damian Emanuel Lyimo, Muuguzi Daraja la II (Zahanati ya Mwageni). Bertha Juvenary Nyamwiula, Muuguzi Daraja la II na Nkeshimana Jumanne Kasonga, Muuguzi Daraja la II (Zahanati ya Mwageni B- Mwasungura).

Wengine ni Kissile Nelson Mwakabago, Muuguzi Daraja la II, Eufransia Zacharia Mjuanga, Muuguzi Daraja la II na Ezekiel Christopher Mantyotyo, Tabibu Daraja la II (Co) (Zahanati ya Mwalilo Mnadani). Watumishi wengine ni Thereza Revocatus Lweyemaho, Muuguzi Daraja la II, Kasilda Gervas Nkembo, Tabibu Daraja la II (CO) (Zahanati ya Mwandu Kisesa).

Post a Comment

0 Comments