Ticker

6/recent/ticker-posts

BALOZI MUSHY AKUTANA NA MEYA WA JIJI LA LINZ

Balozi wa Tanzania nchini Austria, Mhe. Celestine Mushy (kushoto)  akutana na kufanya mazungumzo na Meya wa Jiji la Linz, Mhe. Mstahiki Klaus Luger. Balozi alimshukuru kwa mapemzi yake kwa Tanzania ambayo yaliwezesha Jiji la Dodoma kuwa na mahusiano na Jiji la Linz (Sister Cities).   Balozi alimuomba kuimarisha mahusiano hayo zaidi kwa kusainiana makubalino ya ushirikiano kati ya hospitali na vyuo vikuu vya Linz na Tanzania ili kuweza kubadilishana utaalamu, teknolojia, mafunzo, wanafunzi na wahadhiri. Aidha, Balozi alimuomba kuandaa mkutano wa wadau wote ili aweze kuongea nao. Mhe. Mstahiki Meya alikubali maombi hayo.

Balozi wa Tanzania nchini Austria, Mhe. Celestine Mushy na Meya wa Jiji la Linz, Mhe. Mstahiki Klaus Luger wakiwa katika picha ya pamoja na wasaidizi wao baada ya kufanya mazungumzo.



 

Post a Comment

0 Comments