Ticker

6/recent/ticker-posts

MWENGE WA UHURU 2022 -KUZINDUA,KUWEKA JIWE LA MSINGI MIRADI YA BIL.8.2 SINGIDA, RC SERUKAMBA ANENA MAZITO

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dk. Balozi Batilda Buriani akimkabidhi Mwenge wa Uhuru 2022 Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Peter Serukamba katika Kijiji cha Mseko wilayani Iramba baada ya kuhitimisha mbio zake mkoani humo leo. Mwenge wa Uhuru ukiwa mkoani hapa unatarajiwa kupitia miradi mbalimbali yenye thamani ya Sh.8.2

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Peter Serukamba (katikati) akiwa na viongozi mbalimbali wakati wa makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru. Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida, Alhajj Juma Killimbah, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2022, Sahili Nyanzabara Geraruma na Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dorothy Mwaluko.

Mkufunzi wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Kapteni Mussa Mohamed Ngomambo (katikati) akiwa na wakimbiza Mwenge wa Uhuru 2022.
Mkufunzi wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Kapteni Mussa Mohamed Ngomambo, akiwa na Wakuu wa Wilaya za Singida. Kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda, Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Sophia Kizigo na Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mhandsi Paskas Mragili.




Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Peter Serukambaakimkabidhi Mwenge wa Uhuru 2021 Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleimani Mwenda kwa ajili ya kuanza mbio zake wilayani humo.
Viongozi mbalimbali wakiwa katika mapokezi ya Mwenye wa Uhuru.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dorothy Mwaluko na Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda akionesha furaha zao wakati wa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru.
Wananchi wa Wilaya ya Iramba wakiwa kwenye mapokezi hayo ya Mwenge wa Uhuru.
Mwenge wa Uhuru ukipokelewa.
Vijana wa Hamasa kutoka Mkoa wa Tabora wakinogesha mapokezi ya Mwenge wa Uhuru kwa kucheza.
Vijana wa Skauti wakiwa tayari kwakuupokea Mwenge wa Uhuru.
Wananchi wakiwa katika mapokezi hayo.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye mapokezi hayo.
Vijana wa Hamasa kutoka Wilaya ya Iramba wakiupiga mwingi kwenye mapokezi hayo.
Kikundi cha Sanaa cha Makhirikhiri kutoka Wilaya ya Iramba kikitoa burudani.
Vijana wa Hamasa kutoka Mkoa wa Tabora wakitoa burudani.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Peter Serukamba na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Sophia Kizigo wakiwa kwenye mapokezi hayo.
Mkurugenzi wa Halmashauri Ya Wilaya ya Mkalama, Asia Mesos (kushoto) na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida Ester Chaula wakiwa kwenye mapokezi hayo.
Mapokezi hayo yakiendelea.
Wenyeviti wa Halmashauri za Wilaya za Manyoni, Singida na Ikungi wakiwa kwenye mapokezi hayo ya Mwenge wa Uhuru.
Wakimbiza Mwenge wa Uhuru 2022 wakiwa kwenye mapokezi hayo. Kutoka kushoto ni Rodrick Ndyamukama, Emmanuel Chacha, Gloria Peter, Zadida Abdallah Rashid na Ali Juma Ali.
Itifaki za Mwenge wa Uhuru na Dua zikifanyika.
Vijana wa Skauti wakimvika Skafu Mkimbiza Mwenge wa Uhuru, Gloria Peter ikiwa ni ishara ya kumkaribisha Mkoa wa Singida tayari kwa kuukimbiza Mwenge wa Uhuru 2022.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2022, Sahili Nyanzabara Geraruma akizungumza wakati akiwaaga Wana Tabora baada ya kuukimbiza Mwenge wa Uhuru katika mkoa huo.
Vijana wa Skauti, Joseph Paul (kulia) na Michael Elibariki (kushoto) wakimvika Skafu Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2022, Sahili Nyanzabara Geraruma ikiwa ni ishara ya kumkaribisha Mkoa wa Singida kukimbiza mwenge huo.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2022, Sahili Nyanzabara Geraruma (kushoto) akisalimiana na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida (CCM) Martha Gwau wakati wa mapokezi wa Mwenge wa Uhuru 2022.
Vijana wa Skauti wakionesha ukakamavu wakati wa mapokezi hayo.


Mratibu wa Mbo za Mwenge wa Uhuru 2022 Mkoa wa Singida, Fredrick Ndahani akiwaelekeza jambo waratibu wa Mwenge huo ngazi za Wilaya wakati wa mapokezi hayo.
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakiimarisha ulinzi wakati wa mapokezi hayo.
Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dorothy Mwaluko akiwa ameushika Mwenge wa Uhuru wakati wa mapokezi hayo.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida (CCM) Martha Gwau akiwa ameushika Mwenge wa Uhuru 2022 wakati wa mapokezi hayo..




Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Singida (CCM) Ahmed Kaburu akiwa ameushika Mwenge wa Uhuru 2022 wakati wa mapokezi hayo..
Msatahiki Meya wa Manispaa ya Singida, Yagi Kiaratu akiwa ameushika Mwenge wa Uhuru 2022 wakati wa mapokezi hayo..


Waandishi wa Habari Mkoa wa Singida wakiwajibika wakati wa mapokezi hayo ya Mwenge wa Uhuru.
Viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakiwa kwenye mapokezi hayo.
Mapokezi ya Mwenge wa Uhuru yakiendelea upande wa Wilaya ya Iramba.
Taswira ya mapokezi hayo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Michael Matomora akiwa ameushika Mwenge wa Uhuru 2022 wakati wa mapokezi hayo..
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Hussein Sepoko akiwa ameushika Mwenge wa Uhuru 2022 wakati wa mapokezi hayo..

**************************

Na Dotto Mwaibale, Singida


MWENGE wa Uhuru umepokelewa leo (Agosti 9, 2022) mkoani Singida ukitokea mkoa wa Tabora ambapo ukiiwa Singida utazindua na kuweka jiwe la msingi kwenye miradi yenye thamani ya shilingi 8,280,426,339.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, akitoa taarifa ya mkoa wakati wa kupokea Mwenge wa Uhuru katika kijiji cha Mseko wilayani Iramba, alisema katika utekelezaji wa miradi hiyo nguvu za wananchi ni Sh.84,203,100,, halmashauri shilingi 173,296,344, Serikali Kuu shilingi 6,449,362,831 na wahisani shilingi 1,575,742,564.

Ifuatayo ni baadhi ya mambo aliyoyaongea Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Serukamba katika risala yake :-



PONGEZI KWA RAIS SAMIA SULUHU HASSANI

Serikali ya Mkoa wa Singida na wananchi wote tunatoa pongezi kwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa moyo na upendo mkubwa kwa Watanzania hasa katika uboreshaji huduma za afya, barabara, elimu na maji.

Katika kipindi cha uongozi Awamu ya Sita Mkoa wa Singida umepokea jumla ya shilingi 270,371,690,554.00 kutoka Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, Wadau mbalimbali wa kwenye miradi ya Maendeleo katika sekta Elimu, Afya, Utawala, Kilimo, Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Sekta Ya Barabara, Nishati, Maji, Habari Na Mawasiliano.

Katika sekta ya Elimu jumla ya shilingi 30,571,875,316.74 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya miundombinu ya Elimu pamoja na utoaji wa Elimu Bila Malipo.

Jumla ya madarasa 236 yamepatiwa fedha za ukamilishaji na madarasa mapya 801 yamejengwa, jumla ya matundu ya vyoo 827 yamejengwa, jumla ya maabara 83 zimekamilishwa na ujenzi wa mabweni 4,.

Sekta ya Afya jumla ya shilingi 28,407,068,716.19 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali 4, vituo vya afya 15 na ujenzi wa zahanati utoaji wa chanjo na ujenzi wa vyoo katika vituo vya kutolea huduma za afya.

Katika eneo la Utawala jumla ya shilingi 5,090,191,781.28 zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba 23 za watumishi na ujenzi wa majengo 3 ya Ofisi.

Katika Sekta ya Kilimo jumla ya tani 486.773 za mbegu za alizeti zenye ruzuku ya Serikali ya thamani ya shilingi 2,260,755,000.00 zilitolewa kwa wakulima wa Mkoa wa Singida zilitolewa.

Kwenye eneo la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi jumla ya shilingi 12,076,417,785.08 zilitolewa kupitia TASAF III kwa kaya maskini na fedha zilizokopeshwa kwa vikundi 409 vya wanawake na vijana na watu wenye ulemavu.

Sekta ya Nishati imewezeshwa kutekeleza miradi yenye thamani ya shilingi 63,507,622,522.00 ya umeme ili kukamilisha vijiji 176 vya Mkoa wa Singida ambavyo havijafikiwa na umeme.

Sekta ya Barabara jumla ya miradi yenye thamni ya shilingi 97,690,067,211.00 imetekelezwa na mingine inaendelea kutekelezwa kujenga madaraja, matengenezo madogo na ujenzi wa barabara kaatika Mkoa wetu, vilevile Mkoa kupitia sekta ya Habari na Mawasiliano ulipatiwa shilingi 816,292,481.00 kuweka anwani za makazi .



Uongozi wa Mkoa na wananchi wote wa Singida tunamuunga Mkono Rais kwa kufanya kazi kwa bidii, kuthamini rasilimali zetu na kuzitumia kwa uaminifu mkubwa ili kuleta maendeleo yenye tija kwa Taifa letu. Tunaomba Mwenyezi Mungu ampe afya njema ili kazi iendelee!



SENSA YA WATU NA MAKAZI



Mwaka huu Taifa letu litatekeleza zoezi muhimu la Sensa ya Watu na Makazi, Mkoa wa Singida umejipanga kuhakikisha zoezi hili linafanikiwa.

Maandalizi ya Sensa 2022 yamefanyika ambayo yanajumuisha Utengaji wa maeneo 2,501 yametengwa kama ifuatavyo; Singida Mjini (295), Manyoni (279), Itigi (173), Ikungi (539), Singida Vijijini (434), Mkalama (388) na Iramba (393).

Uundaji wa Kamati za Sensa, Sensa ya Majaribio, Ajira za Makarani, kufanya mafunzo ngazi ya Mkoa na Mafunzo kwa wasimamizi ngazi ya II (Mkoa) yamekwisha fanyika.

Aidha mafunzo ngazi ya III ambayo yalianza rasmi tarehe 31 Julai 2022 hadi 19 Agosti 2022 kufundisha wasimamizi na makarani wa Sensa .

Moja ya maandalizi ya Sensa ni pamoja na kukamilisha ajira za muda za Makarani na Wasimamizi wa Sensa na kuanza mafunzo tarehe 31 Julai 2022 ngazi ya Wilaya.

Jumla ya makarani na wasimamizi wa Sensa wapatao 5,449 wameajiriwa katika Mkoa ikiwa ni kipaumbale kwa vijana wasio na ajira.

Ili kufanikisha zoezi la Sensa, Kamati za Sensa katika ngazi zote za kiutawala zimeundwa na zimefanya kazi ya elimu ya Sensa na kugawa vipeperushi maeneo mbalimbali.

Mkoa umepokea takribani vipeperushi 30,000 ambavyo vilisambazwa kwenye Halmashauri zote ili kuwafikia wananchi,uhamasihaji wa ushiriki wa wananchi katika Sensa unaendelea kufanyika kupitia mikutano ya hadhara,vyombo vya habari,mitandao ya kijamii pamoja na makongamano.



MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA



Ili kuhakikisha tunatokomeza na kumaliza kabisa mizizi ya Rushwa, Mkoa wa Singida unatambua na kupokea ujumbe mwambatano wa:-Mapambano dhidi ya Rushwa, chini ya kauli mbiu, “KUZUIA RUSHWA NI JUKUMU LANGU”.

TAKUKURU Mkoa wa Singida Kipindi cha Mwezi Julai, 2021 hadi Julai, 2022 ilipokea taarifa 238 za vitendo vya rushwa kati ya hizo taarifa 61 zinaendelea na uchunguzi na 22 zilifunguliwa kesi katika mahakama mbalimbali za Mkoa wa Singida.

Aidha,Miradi ya maendeleo ilikaguliwa,elimu ilitolewa kwa wananchi kuhusu madhara ya rushwa kupitia mikutano, Semina , maonesho, vipindi vya Redio vimefanyika kupitia Standard Redio FM na kuimarishwa Klabu za wapinga rushwa katika Shule za Msingi na Sekondari.



HUDUMA ZA AFYA



Mkoa unaendelea na Mapambano dhidi ya Malaria, chini ya kauli mbiu “Ziro Malaria Inaanza na Mimi nachukua hatua kuitokomeza”.

Kiwango cha Maambukizi ya Malaria Mkoa wa Singida ni 2.3%, ukilinganisha na wastani wa kitaifa wa asilimia 7.3 wa maambukizi ya malaria.

Mkoa umelenga kuimarisha maeneo yafuatayo: Kinga, Upimaji na tiba, Ushirikiano na Wadau wa Afya pamoja na kuimarisha mikakati mtambuka.

Eneo la Kinga: Mkoa kwa kushirikiana na OR - TAMISEMI na Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Malaria (NMCP) inatekeleza mpango wa kugawa vyandarua vyenye viuatilifu kupitia shule za msingi za Serikali na Binafsi kwenye Halmashauri sita (6) za Ikungi, Iramba, Itigi, Manyoni, Mkalama na Singida.

Kiasi cha vyandarua 359,757 vinatarajia kugawiwa kwa wanafunzi wote wa shule za Msingi katika kipindi cha Julai hadi Septemba 2022. Aidha, Kwa kipindi cha Januari hadi Juni, 2022 vyandarua vyenye viuatilifu 32,796 (95%) Viligawiwa kwa wajawazito na vyandarua 26,367 (95%) kwa watoto umri chini ya mwaka 1.

Mkoa unaendele kutoa huduma ya chandarua Kliniki kupitia kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya, kutoa elimu kwa kutumia mabango ya kudumu, vyombo vya habari, vituo vya kutolea huduma za Afya na mikusanyiko.

Kutumia fursa zozote za uhamasishaji kuongeza mwitikio wa wananchi kupambana na Malaria kwa kuonyesha matumizi endelevu ya vyandarua.

Eneo la Upimaji na Tiba: Mkoa unaendelea kuimarisha upatikanaji wa dawa Mseto (ALu) na vipimo vya malaria (mRDT) na upimaji wa Malaria kupitia hadubini.

Aidha, upimaji wa Malaria kupitia mRDT na matibabu kwa dawa za malaria (ALu na Sindano ya Artesunate) zinatolewa bila malipo katika Vituo vyote vya kutolea huduma za Afya vya Serikali.

Kwa kipindi cha Januari hadi Juni 2022 jumla ya wagonjwa wateja 137,299 walipimwa malaria ambapo kati yao 10,645 Waligundulika kuwa na vimelea vya malaria na walipatiwa matibabu.

Ushirikiano na Wadau wa Afya: Mkoa unaendelea kushirikisha Viongozi wa dini, Viongozi wa kisiasa, Sekta binafsi kutekeleza Afua mbalimbali zinazo lenga kupambana na Malaria.

Mikakati Mtambuka: Mkoa unaendelea kuhamasisha wananchi kujiunga na Bima ya Afya ili kukabiliana na gharama za matibabu.




MAPAMBANO YA DAWA YA KULEVYA




Mapambano dhidi ya Dawa za kulevya, chini ya kauli mbiu; “Tuelimishane juu ya Tatizo la Dawa za Kulevya, Kuokoa Maisha”.

Mkoa umejipanga kuendelea kutoa elimu kuhusu madawa ya kulevya na athari zake kwa jamii kupitia shule, vikao, mikutano, maadhimisho mbalimbali yanayofanyika ngazi za Halmashauri, Mkoa na vyombo vya habari vilivyopo ndani ya Mkoa.

Vituo vya kutolea huduma za Afya vinatoa huduma kwa waathirika wa madawa ya kulevya ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya athari za madawa ya kulevya, huduma ya ushauri pamoja na dawa.

Waathirika wa madawa ya kulevya wengi wameathiriwa na bangi, kokaine, ugoro, mirungi na pombe. Kwa kipindi cha mwaka 2021/22 jumla ya wagonjwa 80 wamehudumiwa na kupatiwa matibabu katika vituo vya kutolea huduma za Afya.

Post a Comment

0 Comments