Ticker

6/recent/ticker-posts

MFUKO WA ELIMU WA TAIFA WATUMIA MILIONI 750 UJENZI WA SHULE YA MTAALA WA KIINGEREZA JIJINI DODOMA.

Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Prof. Maurice Mbago (mwenye Suti ya Bluu) akipata maelezo kuhusu ujenzi wa Shule ya Msingi Msangalale ya Mtaala wa Kiingereza ya jijini Dodoma inajayojengwa kwa ufadhili wa Mfuko wa Elimu wa Taifa unaosimamiwa TEA kwa thamani ya Sh. milioni 750. Jengo la vyumba vinane vya madarasa katika Shule ya Msingi Msangalale ya Mtaala wa Kiingereza ya jijini Dodoma inajayojengwa kwa ufadhili wa Mfuko wa Elimu wa Taifa unaosimamiwa TEA kwa thamani ya Sh. milioni 750.Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Prof. Maurice Mbago (mwenye Suti ya Bluu) akikagua mradi wa ujenzi wa Shule ya Msingi Msangalale ya Mtaala wa Kiingereza ya jijini Dodoma inajayojengwa kwa ufadhili wa Mfuko wa Elimu wa Taifa unaosimamiwa TEA kwa thamani ya Sh. milioni 750.Jengo la utawala katika Shule ya Msingi Msangalale ya Mtaala wa Kiingereza ya jijini Dodoma inajayojengwa kwa ufadhili wa Mfuko wa Elimu wa Taifa unaosimamiwa TEA kwa thamani ya Sh. milioni 750.

Sehemu ya matundu 32 ya vyoo katika Shule ya Msingi Msangalale ya Mtaala wa Kiingereza ya jijini Dodoma inajayojengwa kwa ufadhili wa Mfuko wa Elimu wa Taifa unaosimamiwa TEA kwa thamani ya Sh. milioni 750.

**************************

Shule ya Msingi Msangalale ya mtaala wa Kiingereza inayojengwa kwa ufadhili wa Mfuko wa Elimu wa Taifa unaosimamiwa na Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) inatarajia kuanza rasmi mwezi Januari 2023.

Akitoa taarifa kwa Mwenyekiti wa Bodi ya TEA, Prof. Maurice Mbago aliyetembelea mradi huo unaojengwa katika Kata ya Makulu jijini Dodoma, Mkuu wa Divisheni ya Elimu Awali na Elimu Msingi wa jiji la Dodoama, Prisca Myalla amesema shule itaanza na wanafunzi 320 na itaendelea kuongeza wanafunzi hadi watakapofikia 640 idadi ambayo ni uwezo wa shule hiyo.

Bi Myalla ameongeza mradi huo utasaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi katika shule zenye upungufu wa vyumba vya madarasa, kusogeza karibu na jamii huduma ya elimu na kupandisha ufaulu wa kitaaluma katika Halmashauri ya jiji la Dodoma.

Msanifu Majengo msimamizi wa Mradi huo, Emmanuel Mateo kutoka jiji la Dodoma amesema kwa sasa ujenzi huo unaohusisha jengo la utawala, vyumba vinane vya madarasa na matundu 32 ya vyoo umefikia asiimia 80 ambapo umepangwa kukamilika Novemba 30, 2022.

Mfuko wa Elimu wa Taifa umetoa ufadhili wa Sh. milioni 750 kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo itakayotoa elimu kwa lugha ya kiingereza katika mwaka wa fedha wa 2021/ 2022 kwa lengo la kusaidia jitihada za Serikali za kutoa elimu bora.

Post a Comment

0 Comments