Ticker

6/recent/ticker-posts

RUAHA YAHARIBIWA NA WANANCHI KWA KUVAMIA VYANZO VYA MAJI


Mragibishi na Mdau wa Mazingira Seleman Msindi akizungumza mara baada kufika katika Mto Ruaha Mkuu eneo Ngiliama- Madibira mkoani Mbeya

Sehemu ya mawe hii kwa kipindi hiki cha kiangazi kinakuwa maji lakini hakuna hata tone la maji Bwawa ambalo sehemu ya weusi ni wanyama aina viboko. Bwawa lenye wanyama aina tembo wakiwa wanakunywa maji baada kutoka safari ya mbali kufuata maji.

*************************

*Shughuli za Kilimo na Ufugaji ndio matokeo ya mto Ruaha kukauka

Na Mwandishi wetu

Kituo cha Wanahabari ,Watetezi wa Rasilimali na Taarifa (MECIRA) kimesema kuwa athari za Hifadhi ya Ruaha ni matokeo ya shughuli za kibinadamu kuingia katika hifadhi hiyo.

Adhari hiyo imesababishwa na bonde la usangu -Ihefu wananchi kuvamia hifadhi kuendesha kilimo na ufugaji na kuathiri mto Ruaha kushindwa kutirisha maji na madhara yake yanaonekana kwa wanyama kutegemea mabwawa katika mto huo.

Kituo cha Wanahabari ,Watetezi wa Rasilimali na Taarifa (MECIRA)kilitembea sehemu moja ya mto Ruaha Ngeliama iliyopo Kata Madibira ya Madibira wilayani Mbarali mkoani Mbeya (Bonde la Usangu) na kuona namna mto Ruaha ukiwa umekauka kutokana na eneo kubwa ya uhifadhi kuingiliwa na shughuli za kilimo ,Ufugaji pamoja na uvuvi na kusababisha maji kushindwa kufika katika mto huo. Akizungumza katika hifadhi ya Ruaha Mragibishi na Mdau wa Mazingira Msanii Selaman Msinde 'Afande Sele' amesema Mto Ruaha na hifadhi ya Ruaha sasa inakabiliwa na ukame kutokana vyanzo vya maji kukauka katika mto huo ambapo kumesabishwa na mikono ya wanadamu.

Msindi amesema kuwa katika maoneo waliyopita kumekuwa na mashamba makubwa yaliyoko katika hifadhi huku wakulima wakiona ni haki yao kuendesha kilimo ,ufugaji pamoja na ukataji miti.

Amesema kuwa baada ya kupeleleza katika vijiji vilivyopo ndani ya hifadhi ambapo kuna vijiji havijihusishi na kilimo wa ufugaji hapo ni kujiuza wanafanya nini wakati kuna ujangili ambapo ni nani anafanya hivyo hayo maswali yote changamoto kwenye jamii.

Msindi amesema kuna ripoti mbalimbali katika vijiji vilivyopo ndani ya hifadhi watu wanakamatwa na silaha za kivita lakini vizingizio vilivyopo wanasema wanafanya kilimo.

Amesema kuwa Mto Ruaha na Mbuga ya Uhifadhi inatakiwa jamii na watunga sera kuangaliwa kwa ukaribu sana na kupata utashi wa kisiasa katika kukabilina.

Aidha amesema wanyama wanatembea umbali mrefu kutafuta maji ambapo kwa sasa yamebaki mabwawa hivyo mabwawa yakikauka wanyama wataenda wapi.

Amesema kwa sasa kuna changamoto ya nishati ya umeme ambayo imesababishwa na maji kupungua kwa kiwango kikubwa kwenye mto Ruaha.

Afande Sele anasema Mto Ruaha unapeleka maji katika vituo vya kuzalisha Umeme ambavyo ni Kidatu ,Mtera pamoja na Kihansi lakini kwa sasa uzalishaji wake unapungua kila siku.

Amesema kuwa uchumi wa unatagemea nishati ya umeme kwa kwa watu zaidi milioni 61 kwa mujibu wa sensa ya mwaka huu hivyo kunahitaji kulinda mto huo pamoja na Ikolojia ya Uhifadhi ya Mbuga ya Ruaha na Selous.

Msindi amesema mto Ruaha kwa sasa hatarini kukauka kwa kipindi kifupi baada ya Masika kutokana sehemu vyanzo vidogo vidogo kushindwa kuingiza maji katika mto mkuu Ruaha.

Amesma Kwa mujibu wa Ripoti mbalimbali zinaeleza mto Ruaha ndio sehemu kubwa ya uzalishaji wa Nishati Umeme huku kuwa chanzo kikubwa katika cha maji kwenye Bwawa la Nyerere na kufuatia utunzaji wa Ikolojia katika hifadhi Selous na Ruaha.

Hifadhi ya Ruaha na Selous na ndio hifadhi kubwa zenye makundi ya wanyama wanaotembea kwa pamoja hivyo kukosekana na kwa maji ni hatari wanyama hao wakafa au kuondoka kutokana na kukosekana kwa maji.

Post a Comment

0 Comments