Ticker

6/recent/ticker-posts

JENGENI UADILIFU KWA WANATAALUMA SEKTA YA ARDHI KUEPUKA DHURUMA NA RUSHWA KWA KIZAZI KIJACHO-DKT MABULA

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula katikati na Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kushoto pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Cha Ardhi Tabora Dkt. Lucy Shule wakiwa katika ya pamoja na Wajumbe wapya wa Bodi ya Chuo cha Ardhi Tabora. Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula akisoma ujumbe wa jiwe la Msingi mara baada ya kufungua jengo la miadhara kwa ajili ya wanafunzi wa Chuo cha Ardhi Tabora uku Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Allan Kijazi akifuatilia kwa makini. Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Allan Kijazi akitoa maneno ya utangulizi kabla ya kumkaribisha Wiziri Angeline Mabura kuzindua Bodi ya Chuo cha Ardhi Tabora. Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akimkabidhi vitendea kazi Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Cha Ardhi Tabora Dkt. Lucy Shule jana Mkoani Tabora. Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akimkabidhi vitendea kazi Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Cha Ardhi Tabora Bw. Seushi Mburi jana Mkoani Tabora.

********************

Na Anthony Ishengoma

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ameitaka Bodi ya Chuo Cha Ardhi Tabora inayosimamia maendeleo ya taaluma Chuoni hapo kuhakikisha mitaala ya Chuo hicho inalenga kutoa elimu sahihi itakayowaandaa wahitimu wake kuwa watumishi waadilifu watakaopiga vita uonevu, migogoro, udanganyifu, dhuruma na rushwa katika Sekta ya ardhi Nchini.

Waziri Mabula amesema hayo jana alipofika Chuo cha Ardhi Tabora kwa lengo la kuzindua Bodi mpya ya Chuo hicho na kuongeza kuwa uadilifu kwa wanafunzi unatakiwa kujengwa kwa wanachuo wanaosomea taaluma ya masuala ya ardhi ili hapo baadae waweze kuwa watumishi waadilifu kwa wananchi ukizingatia ardhi ni sehemu ambayo mahitaji yake ni makubwa hapa nchini.

Dkt. Mabula ameihakikishia bodi hiyo mpya kuwa kadri itakavyowezekana, Wizara yake itawapa kila aina ya ushirikiano kwa kutoa miongozo na mahitaji yote muhimu kwa wakati kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao ya kukisimamia na kukiendeleza Chuo ili kiweze kuendelea kuleta manufaa nchini.

‘’Kuhusu changamoto zinazokikabili Chuo, Serikali kupitia Wizara yangu inaendelea kutekeleza mipango mbalimbali kwa kujenga miundombinu mipya na kukarabati iliyokuwepo kulingana na upatikanaji wa fedha’’. Aliongeza Dkt. Angeline Mabula, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Waziri Mabula aliongeza kuwa Ujenzi wa maktaba kubwa ya kisasa inayokaribia kukamilika, ni moja ya utekelezaji wa mipango hiyo na nia thabiti ya Wizara katika kuzikabili changamoto ni kuongeza ufanisi kitaaluma.

Waziri Mabula aliongeza kuwa Wizara itaendelea kuongeza idadi ya watumishi hasa wakufunzi na kuhakikisha pia Chuo kinapatiwa vifaa na mitambo ya kufundishia na kujifunzia ili kiweze kutoa mafunzo yanayokidhi viwango.

‘’Ni ukweli usiopingika kuwa mafunzo yakitolewa kwa viwango vinavyohitajika, tutapata wahitimu wenye ubora katika fani zao utakaowawezesha kufanya kazi kwa kujiamini na kwa ufanisi mkubwa’’. Aliongeza Waziri Mabula.

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Allan Kijazi aliwaambia wajumbe wapya ya bodi hiyo kuwa moja ya kazi yao ni kuhakikisha wanakiendesha chuo kwa kuzingatia maendeleo ya yaliyopo hususani madiliko ya kidigitali yanayotumika kwasasa duniani.

Dkt. Allan Kijazi aliongeza kuwa kwasasa dunia inaendesha uchumi wake kwa maendeleo ya sayansi na teknlojia hivyo mitaala ya chuo hicho inatakiwa kuangalia upya ili kuendana na maendeleo ya kiteknolojia yaliyopo.

‘’Hatuwezi kuendelea na mipango ileile ya miaka kumi na tano iliyopita hivyo ni lazima tubadilike ili kuendana na mabadiliko yaliyopo kwani muhimu kukivusha chou ili kiendane na uchumi wa kidigitali kwa kuwafundisha wanafunzi masomo ya utawala wa ardhi yanayoendeshwa kidijitali.’’ Aliongeza Dkt. Allan Kijazi.

Naye Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Ardhi Tabora Dkt. Lucy Shule alihaidi kuyafanyia kazi mapungufu yaliyopo lakini pia kuendeleza mazuri ya Bodi iliyopita ili kuleta mafanikio ambayo yeye na Bodi yake watayapuitia na kuyafanyia kazi.

Chuo cha Ardhi Tabora kinapokea Bodi mpya ya chuo hicho inayundwa na Wajumbe tisa ambayo imeteuliwa hivi karibuni na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabura na imeanza kazi jana baada ya kuzinduliwa na Waziri huyo.

Post a Comment

0 Comments