Ticker

6/recent/ticker-posts

KAMPENI YA KUPINGA RUSHWA YA NGONO YAZINDULIWA...RPC ASISITIZA UJASIRI KUKATAA RUSHWA YA NGONO


Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akizungumza wakati akizindua Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs. Picha na Kadama Malunde
Waendesha Baiskeli wanawake wanaokimbia na ndoo kichwani wakichuana wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs. 
Waendesha baiskeli kundi A la wanaume wakichuana vikali wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.

Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi amezindua Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono yenye kauli mbiu ‘ Kuwa Jasiri Kataa Rushwa ya Ngono’ inayoendeshwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Karibu Tanzania Organization (KTO) kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na Vyuo 54 vya Maendeleo ya Wananchi (FDCs).

Uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono umefanyika leo Jumamosi Desemba 17,2022 katika uwanja wa CCM Kambarage Mjini Shinyanga ukiambatana na utoaji wa elimu ya Rushwa ya Ngono kwa njia ya michezo ya Baiskeli ambapo wanamichezo wa mbio za baiskeli kupitia Chama Cha Mbio za Baiskeli Mkoa wa Shinyanga wameshindana na kuondoka na zawadi mbalimbali.

Miongoni mwa mbio za baiskeli zilizofanyika ni mbio za wanawake wanaokimbia na ndoo za maji kichwani wakizunguka uwanja wa CCM Kambarage, mbio za wanawake kuzunguka uwanja wa CCM Kambarage, mbio za wanaume waliogawanywa katika makundi matatu (A,B,C) kuzunguka uwanja huo na washindi kuanzia namba moja hadi 10 wameondoka na zawadi ya pesa taslimu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni hiyo, Kamanda Magomi amelipongeza Shirika la KTO kwa kuanzisha Kampeni ya Kupinga Rushwa ya ngono likishirikiana na Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi nchini Tanzania (FDCs) na TAKUKURU akieleza kuwa Rushwa ya Ngono inapaswa kupingwa na kila mtu kwani inarudisha nyuma maendeleo ya nchi.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi.

“Rushwa ya Ngono inaanzia nyumbani na kazini ambapo watu wenye mamlaka wanatumia mamlaka yao vibaya wakitaka wapewe rushwa ya ngono ambapo rushwa hii inamuumiza zaidi mwanamke. Huko mtandaoni pia wanawake wanaombwa rushwa ya ngono pale wanapotishiwa picha zao kusambazwa mtandaoni. Rushwa ya ngono inasababisha tupate wataalamu wasio na sifa lakini pia inaua kutokana na kuchangia maambukizi ya magonjwa ya zinaa ukiwemo UKIMWI na inamfanya muathirika wa rushwa ya ngono kuwa mtumwa wa ngono”,amesema Kamanda Magomi.


“Rushwa ya ngono ni unyanyasaji, kunyamazia kimya rushwa ya ngono ni kunyima haki. Kila mtu aguswe na athari za rushwa, kila mmoja apaze sauti. Naomba wananchi mtoea taarifa polisi na TAKUKURU kuhusu vitendo vya rushwa ya ngono na rushwa zingine. Tukipata taarifa hizo tutazishughulikia kwa weledi na usiri mkubwa”,ameongeza Kamanda Magomi.

Kwa upande wake, Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga Bi. Mwamba Masanja amesema rushwa ya ngono siyo fursa ya kujinufaisha na kitu/jambo/ huduma hivyo ni lazima kila mmoja anatakiwa kuwa mstari wa mbele kupinga rushwa ya ngono na rushwa zingine kwa ajili ya maendeleo ya nchi.

Mkurugenzi wa Shirika la Karibu Tanzania Organization (KTO) Maggid Mjengwa amesema wanaendesha Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono kwenye vyuo 54 vya Maendeleo ya Wananchi (FDCs) na wameamua kutumia mchezo wa mbio za baiskeli kutoa elimu kuhusu masuala ya rushwa ya ngono ili wawe mabalozi wa kupinga rushwa ya ngono.

“Tupo hapa kwa ajili ya kupinga rushwa ya ngono, KTO tunaamini kuwa silaha kubwa ya kupinga rushwa ya ngono ni kujenga uelewa kwa jamii juu ya rushwa ya ngono ndiyo maana hapa leo tunashuhudia mbio za baiskeli. Tunajenga uelewa kupitia michezo Waendesha baiskeli watakuwa mabalozi wa kueneza elimu ya madhara ya rushwa ya ngono. Naomba kila mmoja apinge rushwa ya ngono kwani jambo hili linamhusu kila mwananchi”,amesema Mjengwa.
Waendesha Baiskeli wakitimua vumbi wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono.

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, John Tesha amesema Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inagusa jamii hivyo kuwaomba wananchi kutoa taarifa za vitendo vya rushwa katika jamii.


Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi, Bi. Maria Mkanwa amesema chuo hicho pamoja na vyuo vingine vya maendeleo ya wananchi kwa kushirikiana na KTO wanaendelea kutoa elimu ya kupinga rushwa ya ngono pamoja na kutoa Proramu mbalimbali kwa ajili ya kumwendeleza mwanamke kijana.


Mwakilishi wa Bodi ya KTO, Khalfani Mshana amesema vyuo 54 vya Maendeleo ya Wananchi vimeendelea kushirikiana na KTO na TAKUKURU kutoa elimu ya kupinga rushwa ya ngono kwa kuendesha Programu mbalimbali ikiwemo Programu ya Elimu Haina Mwisho ambayo ni Programu maalumu ya kuendeleza maarifa kwa wanawake vijana waliokatishwa masomo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ujauzito pamoja na wale ambao hawakupata nafasi ya kuendelea na masomo ya sekondari, watasoma masomo ya sekondari kupitia mfumo usio rasmi, masomo ya ufundi, ujasiriamali na stadi za maisha bure.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akizungumza wakati akizindua Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono yenye kauli mbiu ‘ Kuwa Jasiri Kataa Rushwa ya Ngono’ inayoendeshwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Karibu Tanzania Organization (KTO) kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na Vyuo 54 vya Maendeleo ya Wananchi (FDCs) leo Jumamosi Desemba 17,2022 katika Uwanja wa CCM Kambarage Mjini Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akizungumza wakati akizindua Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akizungumza wakati akizindua Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Mwakilishi wa Bodi ya KTO, Khalfani Mshana akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Mwakilishi wa Bodi ya KTO, Khalfani Mshana akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Mkurugenzi wa Shirika la Karibu Tanzania Organization (KTO) Maggid Mjengwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Mkurugenzi wa Shirika la Karibu Tanzania Organization (KTO) Maggid Mjengwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Mkurugenzi wa Shirika la Karibu Tanzania Organization (KTO) Maggid Mjengwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, John Tesha akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, John Tesha akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga Bi. Mwamba Masanja  akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga Bi. Mwamba Masanja  akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi, Bi. Maria Mkanwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Mtoa huduma za kisheria ngazi ya jamii, Anne Deus kutoka kituo cha Msaada wa Kisheria Community Edivication Organization (CEO) akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Waendesha Baiskeli kundi C wakishindana mbio wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Waendesha Baiskeli kundi C wakishindana mbio wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Waendesha Baiskeli wanawake wanaokimbia na ndoo kichwani wakijiandaa kuanza mbio wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Waendesha Baiskeli wanawake wanaokimbia na ndoo kichwani wakichuana wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Waendesha Baiskeli wanawake wanaokimbia na ndoo kichwani wakichuana wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Mwendesha Baiskeli maarufu Makirikiri akishangilia baada ya kushika nafasi ya kwanza kundi la wanawake wanaokimbia na ndoo kichwani wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Waendesha Baiskeli kundi B wakitimua vumbi wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.

Mwendesha Baiskeli Paul Maiga akishangilia baada ya kushika nafasi ya kwanza kundi B la Wanaume wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.

Wanafunzi wa Chuo cha Buhangija FDC wakitoa burudani ya Igizo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Wanawake waendesha baiskeli bila ndoo kichwani wakitimua vumbi wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.

Mwendesha Baiskeli maarufu Futi Mbili akishangilia baada ya kushika nafasi ya kwanza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Vijana wa kundi la Kambi ya Nyani wakitoa burudani wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Waendesha baiskeli kundi A la wanaume wakichuana vikali wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Waendesha baiskeli kundi A la wanaume wakichuana vikali wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Waendesha baiskeli kundi A la wanaume wakichuana vikali wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs.
Waendesha baiskeli kundi A la wanaume wakihitimisha mbio baada ya kuzunguka uwanja wa CCM Kambarage mara 35 wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Rushwa ya Ngono inayoendeshwa na Shirika la KTO kwa kushirikiana na TAKUKURU na FDCs. Kulia ni Mshindi wa kwanza George Izengo
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akikabidhi zawadi ya shilingi 50,000/=  Mwendesha Baiskeli Makirikiri baada ya kuibuka mshindi wa kwanza mbio za baiskeli huku umebeba ndoo ya maji kichwani kuzunguka uwanja wa CCM Kambarage mara 15
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akikabidhi zawadi ya shilingi 50,000/=  Mwendesha Baiskeli Futi Mbili baada ya kuibuka mshindi wa kwanza mbio za wanawake kuzunguka uwanja wa CCM Kambarage mara 15
Zawadi zikiendelea kutolewa kwa washindi
Zawadi zikiendelea kutolewa kwa washindi
Zawadi zikiendelea kutolewa kwa washindi
Zawadi zikiendelea kutolewa
Zawadi zikiendelea kutolewa 
Zawadi zikiendelea kutolewa
Wadau wakifuatilia burudani uwanjani
Wadau wakifuatilia burudani uwanjani
Wadau wakifuatilia burudani uwanjani
Wadau wakifuatilia burudani uwanjani
Wadau wakifuatilia burudani uwanjani
Wadau wakifuatilia burudani uwanjani
Wadau wakifuatilia burudani uwanjani
Wadau wakifuatilia burudani uwanjani.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Post a Comment

0 Comments