Ticker

6/recent/ticker-posts

MADJS WA DAR KUUWASHA MOTO CLUB BEN BISTRO LOUNGE TANGA MKESHA WA MWAKA MPYA

Meneja wa Club Benbistro Hamisi Hassan akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusu walivyojipanga kuaga mwaka 2022 na kuukaribisha mwaka 2023 kwa staili ya aina yake ikiwemo kuwashukuru wateja wao kushoto ni Marton wa Club hiyo Sarah Patrick
Meneja wa Club Benbistro Hamisi Hassan akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusu walivyojipanga kuaga mwaka 2022 na kuukaribisha mwaka 2023 kwa staili ya aina yake ikiwemo kuwashukuru wateja wao kushoto ni Marton wa Club hiyo Sarah Patrick
Marton wa Club hiyo Sarah Patrick akizungumza namna walivyojipanga kushoto ni Msimamizi wa Club hiyo Silvester Kasembe
Marton wa Club hiyo Sarah Patrick akizungumza namna walivyojipanga kushoto ni Msimamizi wa Club hiyo Silvester Kasembe

Msimamizi wa Club Ben Bistro Lounge Silvester Kasembe


Na Oscar Assenga,Tanga.

MADJS Maarufu kutoka Jijini Dar es Salaam na wakishirikiana na wenyeji wa Jiji la Tanga wanatarajia kuuwasha moto Club Maarufu Jijini Tanga “BEN BISTRO” siku ya mkesha wa kuuaga mwaka 2022 na kuukaribisha mwaka 2023 kwa staili ya aina yake ikiwemo kuwashukuru wateja wao

Akizungumza leo na waandishi wa Habari Jijini Tanga Meneja wa Benbistro Hamisi Hassan alisema kwamba burudani hizo zitaanza siku ya kuuaga mwaka na kuukaribisha mwaka 2023 na wamejiandaa kikamilifu kuhakikisha wateja wao wanapata burudani kali.

Alisema kwamba Pamoja na uwepo wa burudani hizo lakini wanawashukuru wateja na wadau wao tokea walipoanza mpaka sasa na kikubwa wamejiandaa kikamilifu na vitu ni vingi upande wa jikoni na club huku akieleza watahakikisha pia usalama unaimarishwa lengo kuwawezesha wadau wao na wateja kusheherekea mwaka mpya

“Kikubwa ni shukrani kwa wateja wetu na wadau wanaotusapoti tokea tumeanza mpaka sasa na tunawaambia mkesha wa Jumamosi na Jumampili kutokuwa na burudani kutoka kwa madjs kutoka Dar na tunaufunga mwaka “Alisema

Aidha alisema kwamba wanawahaidia wateja wao kuendelea kuboresha huduma zao ikiwemo kuhakikisha suala la usalama wao linaendelea kuwepo kila wakati na muda wote.

Awali akizungumza Mdau wa Club Benbistro Kamafa Forever alisema kwamba uwepo wa Club hiyo ambayo imekuwa tofauti na zile za awali umewasaidia wapenda burudani Jijini Tanga kupata ladha za uhakika ambazo hapo awali walikuwa wakizikosa

“Kinachofanyika Club Benibistro ni spesho sana na sehemu nzuri ambayo wadau wa burudani wataendea kupata burudani ya kuufunga mwaka na sababu za kupeleka uwepo wa madjs wapya ni kupata ladha tofauti ambazo zitakuwa na vionjo vya aina yake “Alisema

Naye kwa upande wake Matron wa Club hiyo Sarah Patrick alisema kwamba upande wa huduma ipo vizuri sana na wamejipanga kuhakikisha wanawahudumia wateja wao kama ilivyokuwa kawaida na kuhakikisha hakuna mtu ambaye anakosa vinywaji kutokana na aina ya wahudumu wachangamfu waliopo.

Hata hivyo msimamizi wa Club hiyo Silvester Kasembe alisema kwamba mwaka 2023 wanatarajia kufanya mambo makubwa Zaidi na sehemu hiyo ni nzuri ya Kwenda kupata burudani hivyo wanawakaribisha wateja wao kutoka ndani na nje ya Jiji la Tanga.


Post a Comment

0 Comments