Ticker

6/recent/ticker-posts

VIKUNDI VYA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU WAPATIWA PIKIPIKI NA BAJAJI MANISPAA YA SHINYANGA


Awali Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko (wa pili kushoto) akiwa amepanda pikipiki hizo.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akikabidhi funguo kwa mwendesha bodaboda. Kulia ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akifuatiwa na Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias Ramadhan Masumbuko.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga imekabidhi Mikopo ya Shilingi Milioni 144.4 kwa vikundi 9 vya Vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kwa kuwakabidhi vitendea kazi zikiwemo pikipiki 34 na Bajaji tatu kwa ajili ya biashara ya usafirishaji.


Akizungumza wakati wa kukabidhi Pikipiki na Bajaji leo Ijumaa Desemba 2,2022 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema amewataka wanufaika wa mikopo hiyo kurejesha mikopo hiyo kwa wakati na kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali.

“Vijana tumewapatia pikipiki hizi hakikisheni mnazitumia kujiingizia kipato kama ilivyokusudiwa. Tayari mna leseni na Pikipiki na bajaj hizi zimekatiwa bima kubwa. Msitumike na wahalifu na fuateni sheria za usalama barabarani, msipakize watu zaidi ya mmoja kwenye pikipiki ‘mshikaki’ na msibebe mizigo mikubwa”,amesema Mkuu huyo wa mkoa.


Aidha amesema pia anataka kuwepo kwa Kanzi Data ‘Data Base' ya waendesha pikipiki mkoa mzima wa Shinyanga ili kuwatambua waendesha bodaboda wote kubaini wasio waaminifu wanaoshiriki vitendo vya uhalifu.

“Hongera sana Manispaa ya Shinyanga kwa kuendelea kutoa mikopo kwa vijana,wanawake na watu wenye ulemavu ambapo tangu mwaka 2015 mpaka mwaka 2022 mmefanikiwa kutoa zaidi ya Shilingi Bilioni 1.5. Naomba muendelee kutoa mikopo ili wananchi waweze kuinuka kiuchumi”,amesema Dkt. Mjema.

Amesema Serikali mkoani Shinyanga inaendelea kuboresha miundombinu ikiwemo ujenzi wa Stendi na barabara ili kuboresha maisha ya wananchi.

“Sasa hivi Shinyanga kuna Vibe kubwa!! Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga anajitahidi kuibadilisha Manispaa ya Shinyanga. Tunatengeneza miundo mbinu hapa ili muwe mnatereza tu…ukiingia mjini hakuna vumbi na tayari tumeanzisha usafiri wa Hiace kwenye baadhi ya maeneo hapa mjini Shinyanga na hivi karibuni tutazindua Stendi ya Hiace hapa Kambarage zitakazofanya mizunguko kwenye mitaa mbalimbali mjini Shinyanga”,amesema Dkt. Mjema.

“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan anataka kumgusa kila mwananchi, anataka kuona wananchi wanaondokana na umaskini na ndiyo maana mikopo imeendelea kutolewa”, ameongeza.


Kwa upande wake, Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko amekemea tabia ya baadhi ya waendesha bodaboda kutumiwa na wahalifu huku akiwaonya kuacha kung’oa Vioo vya pikipiki ‘Side Mirror’ na wasiendeshe bila kuvaa kofia ngumu.

Naye Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Shinyanga SSP Debora Lukololo amewakumbusha waendeshaji wa vyombo vya moto kuepuka kuendesha wakiwa wamelewa, wasimame kwenye vivuko ‘Zebra’ na kwenye Taa za barabarani, kutobeba mizigo mikubwa na kutumia lugha nzuri kwa wateja wao.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias Ramadhan Masumbuko amesema wataendelea kutumia mapato ya ndani kwa ajili ya kutekeleza miredi mbalimbali hivyo kuwataka wananchi kuchangamkia mikopo inayotolewa na halmashauri.

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, John Tesha amesema Mikopo hiyo ya shilingi 144,424,000/= ambayo inatokana na Mapato ya ndani imetolewa kwa vikundi 9 vya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu ambao wamenunua pikipiki, bajaji na vifaa vingine vya kutendea kazi huku akiwasisitiza kurejesha mikopo hiyo ili wapatiwe wananchi wengine.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akizungumza leo Ijumaa Desemba 2,2022 katika Stendi Mpya ya Hiace Kambarage Manispaa ya Shinyanga wakati wa hafla ya kukabidhi Mikopo kwa Makundi ya Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu katika Manispaa ya Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akizungumza leo Ijumaa Desemba 2,2022 katika Stendi Mpya ya Hiace Kambarage Manispaa ya Shinyanga wakati wa hafla ya kukabidhi Mikopo kwa Makundi ya Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu katika Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akizungumza leo Ijumaa Desemba 2,2022 katika Stendi Mpya ya Hiace Kambarage Manispaa ya Shinyanga wakati wa hafla ya kukabidhi Mikopo kwa Makundi ya Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu katika Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi Mikopo kwa Makundi ya Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu katika Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi Mikopo kwa Makundi ya Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu katika Manispaa ya Shinyanga.
Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, John Tesha akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi Mikopo kwa Makundi ya Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu katika Manispaa ya Shinyanga.
Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, John Tesha akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi Mikopo kwa Makundi ya Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu katika Manispaa ya Shinyanga.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias Ramadhan Masumbuko akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi Mikopo kwa Makundi ya Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu katika Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi Mikopo kwa Makundi ya Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu katika Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi Mikopo kwa Makundi ya Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu katika Manispaa ya Shinyanga.

Muonekano wa Bajaji kwa ajili ya vikundi vya Watu wenye Ulemavu katika Manispaa ya Shinyanga.
Muonekano wa pikipiki zilizolewa kwa vijana
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akikabidhi funguo za Bajaji kwa mkazi wa Shinyanga. Jumla ya Bajaji tatu zimetolewa kwa makundi ya watu wenye ulemavu
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akikabidhi funguo za Bajaji kwa mkazi wa Shinyanga. Jumla ya Bajaji tatu zimetolewa kwa makundi ya watu wenye ulemavu
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akikabidhi funguo za Bajaji kwa mkazi wa Shinyanga. Jumla ya Bajaji tatu zimetolewa kwa makundi ya watu wenye ulemavu
Mkazi wa Shinyanga akionesha funguo za bajaji, kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema. Jumla ya Bajaji tatu zimetolewa kwa makundi ya watu wenye ulemavu
Mkazi wa Shinyanga akishikana mkono na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema (katikati). Jumla ya Bajaji tatu zimetolewa kwa makundi ya watu wenye ulemavu. Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko.
Mkazi wa Shinyanga akionesha Funguo za Bajaji, katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema, kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko. Jumla ya Bajaji tatu zimetolewa kwa makundi ya watu wenye ulemavu
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akisalimiana na mwendesha bodaboda. Kulia ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko. Jumla ya Pikipiki 34  zimekabidhiwa kwa vijana 34 kupitia vikundi vya vijana 
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akikabidhi funguo kwa mwendesha bodaboda. Kulia ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko. Jumla ya Pikipiki 34  zimekabidhiwa kwa vijana 34 kupitia vikundi vya vijana 
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akizungumza na  mwendesha bodaboda mwanamke bi. Lilian John. Jumla ya Pikipiki 34  zimekabidhiwa kwa vijana 34 kupitia vikundi vya vijana 
Bi. Lilian John akionesha funguo za pikipiki. Jumla ya Pikipiki 34  zimekabidhiwa kwa vijana 34 kupitia vikundi vya vijana 
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akikabidhi hundi ya shilingi 144,424,000/= kwa ajili ya vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu zilizotolewa na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Shinyanga SSP Debora Lukololo akizungumza wakati akikabidhi Viaksi Mwanga kwa ajili ya waendesha bodaboda
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akiwahamasisha waendesha vyombo  vya moto kuzingatia sheria za barabarani.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akizungumza wakati akikabidhi pikipiki kwa waendesha pikipiki 'bodaboda'
Mnufaika wa mikopo ya halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga akitoa neno la shukrani
Waendesha bodaboda wakicheza muziki 
Awali Maafisa wa Jeshi la Polisi wakikagua pikipiki hizo
Awali Maafisa wa Jeshi la Polisi wakikagua pikipiki hizo
Awali Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko (wa tano kushoto) akiwa amepanda pikipiki hizo.
Awali Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko (katikati) akiwa amepanda pikipiki hizo.
Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Shinyanga SSP Debora Lukololo akitoa elimu ya usalama barabarani kwa waendesha bodaboda.
Madiwani na viongozi mbalimbali wakiwa eneo la tukio

Vijana na wanawake wanufaika wa mikopo ya halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga wakiwa eneo la tukio
Vijana na wanawake wanufaika wa mikopo ya halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga wakiwa eneo la tukio.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Post a Comment

0 Comments