Ticker

6/recent/ticker-posts

KITANDULA AKUMBUSHIA FIDIA ZA WANANCHI WALIOPISHA UJENZI WA KIWANDA CHA SARUJI MKINGA



Na Mwandishi Wetu ,Dodoma

MBUNGE wa Jimbo la Mkinga (CCM) Dastan Kitandula ameikumbusha Serikali fidia za wananchi Vijiji vya Kwale na Mtimbwani cha kiasi cha zaidi ya Milioni 570 kwa ajili ya kutoa ardhi kwa ajili ya uwkezaji wa kiwanda cha Saruji cha Hengya kilichokuwa kijengwe wilaya ya Mkinga mwaka 2017.

Kitandula aliyasema hayo Jijini Dodoma wakati wa kikao cha Bunge kinachoendelea ambapo alisema mwaka 2017 alijitokeza Mwekezaji Hengya alionyesha nia ya kuwekeza kwenye sekta ya Sariuji nchini na kiwanda kilikuwa kije kujengwe mkinga na mwaka 2019 Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) ilimpa leseni aje awekekeze.

Alisema kwamba baada ya kupatiwa leseni mwaka 2020 akaanza kutoa fidia kwa ardhi aliyoitwaa kule mkinga wananchi wakaachia maeneo yao tokea wakati huo mpaka leo hakuna fidia stahiki iliyotolewa hivi na kwa sasa wako wananchi 143 wa Mkinga kutoka Kwale na Mtimbwani wanadaiwa Zaidi ya Milioni 570 hazijalipwa.

Alisema kwamba na serikali ilituma timu ikaja kukaa na uongozi wa mkoa na wilaya na mwekezaji wakakubaliana aifanyike kazi ya tathimini isiyo na shaka ili watu hao walipwe na kazi imekamilika na mwekezaji amepelekewa amegoma kulipa viwango stahiki vya kisheria.

Alisema kwamba na hao ni wananchi wamepoteza ardhi zao hawana ruhusa ya kuingia kwenye maeneo hayo mpaka leo hawalipwi kwa nini mwekezaji alipi kwa sababu ana machungu na aliwahi kusema jamani uwekezaji wa hengya ambao wakati ule kama ungefanyika mwekezaji angekuja kiwanda chenye thamani ya Trilioni 2.3 uzalishaji wa saruji alikuwa azalishe tani Milioni 7 kwa mwaka.

Aidha alisema amesikia taarifa ya wizara hapa kwamba leo viwanda 14 vinazalisha tani milioni 10 walikuwa na mwekezaji alikuwa tayari uwekezaji wa tani Trilioni 2.3 azalishe tani milioni 7 kwa mwaka wamemvuruga na alikuja kusema maneno hayo hapo kwamba kuna watendaji hawana nia njema wana wanamvuruga mwekezaji wapo ndani ya viwanda vya saruji.

Alisema wawekezaji hao hawamtaki mwekezaji huyo kutokana na kwamba ataleta ushindani leo wamepoteza uwekezaji huo watu wa Tanga wana machungu wanaiomba Serikali na Waziri Simamia watu wa Mkinga 143 walipwe stahiki zao.

Akizungumzia suala la uuzwaji wa hisa Tanga Cement alisema wao hawapingi lakini wanachokitaka ni kwamba taratibu zifuatwe watu wa Tanga leo hii kuna viwanda 8 baada ya kubinafsishwa vimegueka kuwa magodauni havifanyi kazi, magofu hivyo hawatakuwa tayari kuona Tanga Cementi inabinafishishwa inageuka kuwa godauni au magofui na mtu anakwenda kuchukua malighafi Tanga anakwenda kuzalisha Dar hilo hatutaki .

Mbunge huyo alisema kwamba viwanda 8 wamehangaika ndani ya serikali ili wawekezaji waheshimu mikataba yao wanapokuwa wakiuziwa hiyo ndio hofu yao watu wa Tanga wanaiomba Serikali taratibu za uwekezaji ufanyike wajenga confedence ya wawekezaji kwani hata wanapata shida kwenye sekta madini kila mwekezaji akija anagaganiza kukiwa na dispute waenda kuamuliwa maamuzi hayo nje ya Tanzania .

Alisema kwa sababu wanasema mahakama zetu haziaminika kama kuna jambo limeamulkiwa kisheria tusikiuke maamuzi hayo yaliyoamulkiwa kila mwekezaji anayekuja anakwenda kujisajili kampuni kwenye mikataba ya kimataifa hivyo wakiendelea kukiuka maamuzi.

Post a Comment

0 Comments