Ticker

6/recent/ticker-posts

CCM TANGA YAZICHANGA KARATA ZAKE KUELEKEA KWENYE UCHAGUZI WA 2024/2025

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajabu Abdurhamani akizungumza katika moja ya mikutano yake.

NA Oscar Assenga,TANGA

NDIVYO tunavyosema kusema ili uweze kufanikiwa jambo lolote lile za kisiasa au lingine ni lazima uweke mazingira mazuri mapema kabla ya kulifanya.

Hata wafanyabiashara ambao wanataka kuanzisha shughuli zao lazima wanakwenda kuangalia namna zinafanyika ili baadae wajipange kufungua za kwao tayari wakiwa na uelewa wa kutosha namna ya kuzifanya.

Hali kadhalika katika suala la siasa kila mtu anapoongoza chama Fulani anakuwa na mipango yake dira na muelekeo ambao utampa mafanikio siku za mbeleni kwa kuweka mikakati madhubuti.

Rajabu Abdurhamani ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga ni miongoni mwa viongozi wenye maono makubwa ndani ya chama hicho ambapo baada ya kuchaguliwa Novemba mwaka jana ameanza kufanya kazi kubwa ya kukiimarisha kuanzia ngazi ya vijiji,vitongoji,Mitaa ,Kata na Ngazi ya wilaya.

Katika uimarishaji huo hasa ukizingatia mwakani utafanyika uchaguzi wa Serikali za Mitaa kabla ya ule wa mwaka 2025 ambao utawachagua Rais,Wabunge na Madiwani .

Tayari Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga chini ya Komred Rajabu Abdurhamani kimeanza kimeanza mikakati kabambe ya kuelekea kwenye chaguzi hizo kwa lengo la kuibuka kidedea.

Rajab ambaye awali kabla ya kugombea nafasi hiyo alikuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Pangani ambako nako amefanya mambo makubwa ya kukijenga chama hicho na kusambaratisha upinzania ambapo anaweka bayana kwamba atakitumika chama hicho kwa moyo wake wote kila kujali itikadi za vyama na hilo kwake ndio lilikuwa deni kubwa.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na waandishi wa habari,Rajabu anasema analo deni kubwa kwa wana CCM na wananchi wa Mkoa wa Tanga na vitongoji vyake hasa katika swala zima la kuwaletea maendeleo na kuisimamia Serikali.

Anasema ili kuweza kufikia malengo lazima kujengwe umoja na mshikamano kwa wananchi bila ya kuangalia itikadi za vyama vyao na kuacha malumbano ya kisiasa ambayo hayatakuwa na tija ya kusukuma maendeleo katika Mkoa na wilaya zake.

Anaeleza kwamba Tanga inahitaji maendeleo na kurudisha hadhi yake ya kuwa kitovu cha ajira katika sekta ya viwanda,kilimo na uvuvi na ili kufanikisha azma hiyo Rajabu alisema milango ipo wazi ya kupokea maoni toka kada mbalimbali ili kufanikisha malengo hayo.

Rajabu anasema wakati umefika wa kufanya kazi za chama na kuhakikisha wananchi wanaondokana na kero zinazowakabili kwa kuzitafutia njia sahihi za ufumbuzi wa haraka ili kutekeleza majukumu ya chama hicho kuwasaidia wananchi.

Anasema miongini mwa mambo ambayo wameanza kuyatekeleza ni pamoja na kuanza kufanya ziara ya Mkoa mzima ambapo kuna Wilaya 9, kata 245 na Vijiji zaidi ya elfu kumi sambamba na vitongoji vyake dhamira kubwa kuwafikia wananchi katika maeneo yote na kupata fursa ya kuzungumza nao na kusikiliza kero zao.

Mwenyekiti huyo anasema tayari ameanza kufanya ziara katika Wilaya za Kilindi,Handeni,Pangani na Tanga Mjini ziara iliyojikita hasa kwenye kukiimarisha Chama,kuangalia kero za wananchi na kukagua miradi ya maendeleo.

Katika ziara hiyo Mwenyekiti huyo pia anatoa maelekezo kwa watendaji wa Serikali wanaosimamia miradi ya maendeleo katika maeneo mbalimbali katika Wilaya hizo na kuwaagiza kusimamia miradi hiyo inamalizika kwa wakati na iendane na thamani ya fedha zilizotengwa.

Anasema CCM inawajibu wa kuwasimamia viongozi wa Serikali juu ya utekelezaji wa majukumu yao kwa wananchi na namna wanavyotatua kero kwa mujibu wa kanuni za kazi zao na kufanya hivyo kunaweza kupunguza malalamiko kwa wananchi hao dhidi ya Serikali yao.

“Tuna kazi ya kufanya kwa wananchi wetu na ili kupunguza malalamiko dhidi ya Serikali yao lazima tuwajibike na kuhakikisha tunawatendea haki bila ya kuangalia itikadi za vyama vyao “Anasema Rajabu.

Rajabu anasema si jambo la kawaida kuyafikia maeneo yote ndani ya Mkoa wa Tanga na ni lazima kufanya hivyo ili kubaini changamoto zilizopo na viongozi wa chama wanatakiwa watambue hilo ndilo jukumu la kufanya ziara za mara kwa mara ili kurudisha imani kwa wananchi ambao labda wengi wao walianza kukata tamaa.

Anasema ziara hizo zina tija kwa wananchi hasa wale waishio Vijijini ambapo baadhi ya watumishi wa Serikali wamekuwa na tabia ya kufanya wanavyojisikia katika maeneo yao na badala yake tabia hiyo hupelekea kudumaa kwa maendeleo jambo ambalo katika uongozi wake halitakubalika.

“Mimi na viongozo wenzangu hatutakubali kuona wananchi wanakosa huduma za msingi au miradi ya maendeleo inazorota kutokana na uzembe wa baadhi ya watumishi lazima tuchukue hatua”Anasema Rajabu.

Anasema maendeleo ni mkakati na lazima itengenezewe njia sahihi nya utekelezaji wa maendeleo hayo ambapo Serikali ya ccm imejipambanua kuhakikisha inafikisha huduma zote za kijamii kwa wananchi katika maeneo yao.

Anasema swala sio kufikisha maendeleo katika maeno yote lakini lazima uwepo usimamizi wa kutosha na kuhakikisha miradi na huduma za kijamii zinazotolewa na watumishi wa Serikali vyote kwa pamoja vinafanyika ipasavyo.

Rajabu anasema uwajibikaji na uwadilifu makazini ndio lengo la Serikali ya chama cha mapinguzi na ndio turufu ya ushindi katika chaguzi zijazo jambo ambalo linahitaji kusimamiwa ili chama hicho kiweze kufikia malengo ya kunyakua nafasi zote katika chaguzi zijazo.

Post a Comment

0 Comments