Ticker

6/recent/ticker-posts

WAZIRI KIJAJI:ATAKAYEUZA SUKARI ZAIDI YA 3200 ACHUKULIWE HATUA


Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Dkt Ashatu Kijaji (Mb.) awataka Maafisa Biashara wote nchini kukagua bei ya Sukari duka kwa duka na atakae kutwa na bei zaidi ya shilingi 3,200 achukuliwe hatua za kisheria.

Waziri Kijaji ameyasema hayo alipotembelea Kiwanda cha kuzalisha Sukari cha TPC Mkoani Kilimanjaro kujionea shughuli za uzalishaji na kisikiliza changamoto walizonazo.

Dkt. Kijaji amesema ni jukumu la Maafisa Biashara kutambua mfanyabiashara yeyote atakayeuza sukari juu ya bei kati ya 2800 na 3200 kumchukulia hatua.

Dkt. Kijaji amesisitiza kiwa ni jukumu la Serikali kulinda bidhaa yoyote inayotengenezwa nchini na kufanya Juhudi za kila namna ili kuweza kuwasaidia wawekezaji na wafanyabiashara kuwa na mazingira bora na wezeshi ili kukuza biashara zao na kiwa na tija.

Aidha, amesema bidhaa zinazotengenezwa nchinj zinatakiwa kuwanufaisha wawekezaji na wafanyabiashara wa ndani na biashara yoyotee inayofanyika nje ya nchi inatakiwa kuwa rasmi.

Vilevile amekipongeza Kiwanda cha kuzalisha Sukari cha TPC kwa kutoa ajira zaidi ya elfu 3200 na jinsi kinavojihusisha na utoaji wa huduma kwa jamii inayokizunguka

Naye Kaimu Afisa Mtendaji Utawala wa Kiwanda cha TPC, David Shiltu amesihi watanzania kuwa na Amani kwa kuwa sukari ipo sokoni ya kutosha na hakuna uhaba na uzalishaji unaendelea.

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ,akizungumza na wafanyabiashara wa Mkoa wa Arusha kwa lengo la kusikiliza changamoto walizonazo na kuzitatua

Na.Mwandishi Wetu-ARUSHA

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb.) ameiagiza Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) kuweka kambi Mkoani Arusha kwa lengo la kurasimisha wafanyabiashara wa kilimo ili wapate leseni, tini na vibali vya kusafirisha mazao nje ya nchi.

Dkt. Kijaji ameyasema hayo Agosti 1, 2023 alipokutana na wafanyabiashara wa Mkoa wa Arusha kwa lengo la kusikiliza changamoto walizonazo na kuzitatua

Aidha, Dkt Kijaji amewaonya wafanyabiashara wazawa kuacha mara moja tabia ya kukata leseni na kuwauzia wageni wanaokuja nchini kununua mazao hadi mashambani badala ya kuyafuata kwenye masoko husika

Amesema endapo wafanyabiashara wa mazao wakirasimishwa na kupata leseni zao wataweza kutambulika, idadi yao itajulikana ili kurahisisha jitihada za kuwakwamua kiuchumi wafanyabiashara na wakulima wanauza mazao ya nafaka mbalimbali nchini.

Waziri Kijaji pia amebainisha kuwa Serikali iko mbioni kufuta vibali vya usafirishaji wa mazao vinavyokatwa kila mkoa badala yake kibali kiwe kimoja tu kilicholipiwa kila kitu ili kuwezesha wafanyabiashara wa mazao kubeba mizigo yao na kupelekea mahali husika bila kukata vibali kila Mkoa wanapopita.

Aidha amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita haiko tayari kuwakwamisha wafanyabiashara na wawekezaji kushindwa kufikia malengo yao bali itawasaidia kukua na kuendelea kibiashara, kukaa kwa pamoja na kutatua changamoto zao ili kuhakikisha ufanyaji biashara wao unakuwa na tija na manufaa kwa Taifa .

Dkt. Kijaji amesema ameridhishwa na uwekezaji huo ikiwa ni hatua ya kutatua changamoto ya matumizi ya Vishkwambi katika shule za awali na zile za sekondari ambapo vitasaidia kufundisha wanafunzi namna bora ya kutumia TEHAMA katika mitaala ya elimu

Naye Mkurugenzi wa Kiwanda hicho cha Tanztech Bw. Gurveer Hans amesema Kiwanda hicho kipo tayari kushirikiana na Serikali katika kutoa bidhaa hiyo mashuleni na kwa watu binafsi kwa bei nafuu.

Awali Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wadogo(Machinga) Bi. Amina Samson Njoka akiongea mbele ya Waziri Kijaji amesema wafanyabiashara wadogo katika jiji hilo wamekuwa wakilalamika kuhusu tozo nyingi kutoka OSHA, Jeshi la Zimamoto, Idara ya Uhamiaji pamoja na Halimashauri ambazo zimekuwa kero na kuomba kiwa tozo hizo zitizwe zote mara moja.


Post a Comment

0 Comments