Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Emmerson Mnangagwa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri wa Fedha, Mipango na Maendeleo ya Uchumi wa nchi za Afrika, wa tano kwa waliosimama kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya (aliyemwakilisha Waziri wa Fedha) na wa pili kulia waliosimama ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Dkt. Tausi Kida, baada ya Rais kufungua mkutano wa 56 wa Mawaziri wa Fedha, Mipango na Maendeleo ya Uchumi Afrika (UNECA) uliofanyika Victoria Falls, Zimbabwe.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya akiwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Dkt. Tausi Kida wakielekea Ukumbi wa Elephant Victoria Falls Zimbabwe, wakati wa Mkutano wa 56 wa Mawaziri wa Fedha, Mipango na Maendeleo ya Uchumi (UNECA) uliojadili mikakati ya ukusanyaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya kugharamia shughuli za maendeleo na mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi, ambapo Bw. Mwandumbya alimwakilisha Waziri wa Fedha na Mipango.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya (kulia), ambaye amemwakilisha Waziri wa Fedha katika Mkutano wa 56 wa Mawaziri wa Fedha, Mipango na na Maendeleo ya Uchumi (UNECA) akiteta jambo na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Dkt. Tausi Kida wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, nchini Zimbabwe.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya akiteta jambo na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Dkt. Tausi Kida pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Simon Sirro (kushoto) wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 56 wa Mawaziri wa Fedha, Mipango na Maendeleo ya Uchumi Afrika (UNECA) uliojadili mikakati ya ukusanyaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya kugharamia shughuli za maendeleo na mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi, uliofanyika nchini Zimbabwe.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Dkt. Tausi Kida, akizungumza jambo na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya, wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 56 wa Mawaziri wa Fedha, Mipango na Maendeleo ya Uchumi (UNECA), uliofanyika Zimbabwe.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya (kulia) akisikiliza kwa makini maelezo ya Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Simon Sirro, wakati wa Mkutano wa 56 wa Mawaziri wa Fedha, Mipango na Maendeleo ya Uchumi (UNECA), unaofanyika Victoria Falls, Zimbabwe.
Mawaziri wa Fedha, Mipango na Maendeleo ya Uchumi pamoja na maafisa wengine kutoka nchi za Afrika wakiwa katika Mkutano wa 56 wa Mawaziri hao unaofanyika Victoria Falls, Zimbabwe.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Victoria Falls, Zimbabwe)
0 Comments