Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS AWAAPISHA VIONGOZI MBALIMBALI ALIOWATEUA HIVI KARIBUNI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Ndugu Winfrida Beatrice Korosso kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Ndugu Bibiana Joseph Kileo kuwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Aprili, 2024.
Ndugu Bibiana Joseph Kileo Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka, Ndugu Alice Edward Mtulo Naibu Wakili Mkuu wa Serikali na Ndugu Winfrida Beatrice Korosso Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania wakiapa Kiapo cha Maadili ya Viongozi katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango wakiwa katika picha ya pamoja na Ndugu Bibiana Joseph Kileo Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka, Ndugu Alice Edward Mtulo Naibu Wakili Mkuu wa Serikali na Ndugu Winfrida Beatrice Korosso Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania mara baada ya hafla fupi ya kuwaapisha iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Aprili, 2024.

Post a Comment

0 Comments