Ticker

6/recent/ticker-posts

WAZIRI MKUU AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MWENYEKITI WA KAMATI TENDAJI YA TAASISI YA HUDUMA ZA AGA KHAN

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Mei 3, 2024 amekutana na Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya Taasisi ya Huduma za Aga Khan, Mwana wa Mfalme Bi. Zahra Aga Khan na ujumbe wake, ofisini kwa Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma.

Mheshimiwa Waziri Mkuu amemwambia Kiongozi huyo kuwa Serikali inatambua jitihada kubwa zinazofanywa na Taasisi hiyo hasa katika sekta ya Afya na Elimu na amemuahidi kuwa Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za uwekezaji zinazofanywa na Taasisi ya hiyo.

Post a Comment

0 Comments