Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na Wachezaji wa Timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya Wanaume ya Tanzania ‘Taifa Stars’. Rais Mhe. Dkt. Samia aliwaandalia hafla ya chakula cha mchana na kuwapongeza Wanamichezo waliofanya vizuri Kimataifa, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 10 Januari, 2026. Timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ ilishiriki kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika ‘AFCON’ nchini Morocco na kufika hatua ya mtoano ambayo ni historia kubwa kwa Tanzania tangu ilipoanza kushiriki michunohiyo.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya Jezi ya Timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya Wanaume ‘Taifa Strs’ iliyosainiwa na Wachezaji kutoka kwa Nahodha msaidizi wa Timu hiyo, Bakari Nondo Mamnyeto kwenye hafla ya kuwapongeza iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 10 Januari, 2026.



0 Comments