Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS DKT.HUSSEIN MWINYI ASHIRIKI SWALA YA IJUMAA LEO.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi (kushoto) alipokuwa akiwasalimia Waumini wa Dini ya Kiislamu na Wananchi baada ya kushiriki Swala ya Ijumaa katika Masjid Noor--Abswar Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi "B" Mkoa wa Mjini Magharibi ikiwa ni kawaida yake kushiriki katika Masjid mbali mbali.[Picha na Ikulu] 27/08/2021.

Baadhi ya waumini wa Dini ya Kiislamu walioshiriki katika Swala ya Ijumaa katika Masjid Noor--Abswar Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi "B" Mkoa wa Mjini Magharibi wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani ) alipokuwa akiwasalimia kwa kuwakumbusha masuala ya uwajibikaji.[Picha na Ikulu] 27/08/2021.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi (wa pili kushoto) alipokuwa akisalimia na Mzee wa Msikiti Masjid Noor--Abswar Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi "B" Mkoa wa Mjini Magharibi baada ya kushiriki Ibaada ya Swala ya Ijumaa iliyofanyika leo .[Picha na Ikulu] 27/08/2021.

Post a Comment

0 Comments