Ticker

6/recent/ticker-posts

BALOZI DKT.POSS AFUNGUA MAONESHO YA SANAA ZA UFUNDI AFRIKA MASHARIKI (EASTAFAB )

Dkt.Ally Poss akifungua moanesho ya Sanaa za ufundi Afrika mashariki




Mkurugenzi wa Nafasi arts Space

*****************************

Na Richard Mrusha


Balozi wa Tanzania Nchini Ujerumani Dkt. Ally Poss amezindua maonyesho ya awamu ya kumi ambayo yanahusu Sanaa ya Uchoraji huku akiwataka waandaaji wa maonyesho hayo East Africa Art Biennale Association ( EASTAFAB) kuyafanya yawe na tija zaidi kwa kuhakikisha Sanaa ya Uchoraji iwe fursa ya uchumi kwa Taifa.


Balozi Dkt. Poss amezindua maonyesho hayo katika Kituo Cha Nafasi Arts Space Jijini Dar es Salaam huku akisema kwamba Sanaa ya Uchoraji ni muhimu kwa Jamii kwani inatoa elimu ,kuburudisha kupitia picha ambazo zinachorwa na wasanii wa Uchoraji ambapo pia ni muhimu kwa wanafunzi wa shule za msingi,sekondari na elimu ya juu ambao wanajifunza Mambo mbalimbali kupitia picha.


" Sisi Kama serikali Sanaa ya Uchoraji na Sanaa zingine tutaendelea kuziboreshea mazingira ili wasanii wetu waweze kunufaika na vipaji vyao,serikali imeanzisha mfuko rasmi wa sanaa ambao utazinduliwa Novemba 15 mwaka huu, ambapo utasaidia kutoa mikopo ya riba nafuu ili kuwainua wasanii wetu ambao wanavipaji ili wajiendeleze" amesema Balozi Dkt. Poss ambaye alikua mgeni rasmi katika uzinduzi wa maonyesho hayo.


Kwa upande wake Mwenyekiti na Mwanzilishi wa maonyesho hayo ya East Africa Art Biennale Association ( EASTAFAB) Prof.Elias Jengo amesema kwamba maonyesho hayo yatafanyika kwa muda wa siku 20 ,ambapo mwaka huu yamekua ya awamu ya kumi tangu kuanzishwa kwake mwaka 2003 ikiwa lengo ni kuinua na kuendeleza Sanaa ya uchoraji.


" Tunakushukuru mheshimiwa mgeni rasmi Balozi Dkt. Ally Poss umetoka Dodoma na kushiriki nasi katika uzinduzi wa maonyesho haya ,tutakua pia na kongamano ambalo litawashirikisha wasanii wote ili watoe mawazo yao yatakayosaidia kuinua Sanaa zetu,tutakua na maazimio ambayo tutayawasilisha kwenu serikali muweze kuyafanyia kazi" amesema Prof. Jengo.


Awali Mkurugenzi wa kituo Cha Nafasi Arts Space Rebecca Yeing Ae Mzengi Corey amesema kwamba kituo hicho kitaendelea kuibua vipaji na kuviendeleza ili vijana wengi waweze kujiajiri kupitia vipaji vyao.


Mkurugenzi wa Bodi ya Filam Dkt.Kilonzo kutoka Wizara ya Habari,Sanaa ,Michezo na Utamadunj amesema kwamba wizara hiyo itaendelea kushirikiana na wadau mbalimba katika kuhakikisha Sanaa inakua na kuwafanya wawe na kipato Cha uhakika ambacho kitawasaidia kuendeleza shughuli zao mbalimbali za Sanaa ikiwemo maonyesho.




Mwakilishi wa Ubalozi wa Norwey Nchini Tanzania Annete Otilie pamoja na Mambo mengine amepongeza kuwepo kwa usawa wa kijinsia ambapo wanawake wengi wamekuwa wakipewa nafasi ya kushiriki katika mambo mbalimbali ya Sanaa huku akisisitiza kuwa Norwey itaendelea kusaidia kituo hicho katika kukuza Sanaa.




Wasanii mbalimbali kutoka Tanzania ,Kenya,Uganda na mataifa mengine wameshiriki katika maonyesho hayo huku baadhi yao wamesema kwamba wanaipongeza serikali na wandaaji wa maonyesho hayo katika kuendelea kukuza vipaji vyao.

Post a Comment

0 Comments