Ticker

6/recent/ticker-posts

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYOJIRI LEO BUNGENI JIJINI DODOMA


Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Ecobank, Bw. Charles Asiedu alipomtembelea leo ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma, Novemba 3, 2021


Katibu wa Bunge, Bi. Nenelwa Mwihambi akizungumza na Katibu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Bi. Raya Msellem alipomtembelea leo ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma, Novemba 3, 2021


Katibu wa Bunge, Bi. Nenelwa Mwihambi (kulia) katika picha ya pamoja na Katibu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Bi. Raya Msellem alipomtembelea leo ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma, Novemba 3, 2021


Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge (kushoto) wakiwa katika mazungumzo na Wajumbe wa kamati ya Kinga, Fursa na Maadili ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar (kulia) waliowatembelea kwa lengo la kujifunza jinsi kamati hiyo inavyotekeleza majukumu yake kikao kilichofanyika leo katika ofisi za Bunge Jijini Dodoma, Novemba 3, 2021


Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Mhe. Emmanuel Mwakilasa (kushoto) akimkabidhi Mwenyekiti wa kamati ya Kinga, Fursa na Maadili ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Panya Abdallah kitabu cha makusanyo ya Sheria mbalimbali zinazotumiwa na Bunge tukio lililofanyika leo katika ofisi za Bunge Jijini Dodoma, Novemba 3, 2021


Katibu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Bi. Raya Msellem akichangia jambo wakati kamati ya Kinga, Fursa na Maadili ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar ilipoitembelea kamati ya kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka kwa lengo la kujifunza jinsi kamati hiyo inavyotekeleza majukumu yake tukio lililofanyika leo katika ofisi za Bunge Jijini Dodoma, Novemba3, 2021


Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge wakifuatilia mazungumzo na Wajumbe kamati ya Kinga, Fursa na Maadili ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar waliowatembela kwa lengo la kujifunza jinsi kamati hiyo inavyotekeleza majukumu yake kikao kilichofanyika leo katika ofisi za Bunge Jijini Dodoma, Novemba 3, 2021


Wajumbe kamati ya Kinga, Fursa na Maadili ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakifuatilia mazungumzo na kamati ya kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa lengo la kujifunza jinsi kamati hiyo inavyotekeleza majukumu yake kikao kilichofanyika leo katika ofisi za Bunge Jijini Dodoma, Novemba 3, 2021


Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa kamati ya Kinga, Fursa na Maadili ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar nje ya jengo la Bunge leo Jijini Dodoma, Novemba 3, 2021

(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

Post a Comment

0 Comments