Ticker

6/recent/ticker-posts

MAADHIMISHO YA MIAKA 60 UDSM:MHESHIMIWA YAKUBU AFURAHISHWA NA UKUZAJI WA VIPAJI CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM

NAIBU Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa,Tamaduni na Michezo Mhe.Said Yakubu akimkabidhi hundi ya Shilingi Milioni moja (1,000,000/=) kwa mshindi wa kwanza wa Shindano la Muziki la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Maadhimisho ya Miaka 60 ya Chuo hicho yaliofanyika UDSM tarehe 29/01/2022. NAIBU Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa,Tamaduni na Michezo Mhe.Said Yakubu akimkabidhi hundi ya Shilingi laki saba (700,000/=) mshindi wa pili wa Shindano la Muziki la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Maadhimisho ya Miaka 60 ya Chuo hicho yaliofanyika UDSM tarehe 29/01/2022. NAIBU Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa,Tamaduni na Michezo Mhe.Said Yakubu akimkabidhi hundi ya Shilingi Laki tano (500,000/=) kwa mshindi wa tatu wa Shindano la Muziki la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Maadhimisho ya Miaka 60 ya Chuo hicho yaliofanyika UDSM tarehe 29/01/2022. NAIBU Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa,Tamaduni na Michezo Mhe.Said Yakubu akikabidhi vyeti kwa washiriki wa Mashindano ya Muziki kwenye Tamasha la Muziki la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. NAIBU Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa,Tamaduni na Michezo Mhe.Said Yakubu akizungumza katika Shindano la Muziki la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwenye Maadhimisho ya Miaka 60 ya Chuo hicho yaliofanyika UDSM tarehe 29/01/2022. Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM),Prof.William Anangisye akizungumza katika Shindano la Muziki la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwenye Maadhimisho ya Miaka 60 ya Chuo hicho yaliofanyika UDSM tarehe 29/01/2022.Naibu Makamu Mkuu wa Chuo cha Dar es salaam-UTAFITI Prof.Benadeta Killian akizungumza katika Shindano la Muziki la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwenye Maadhimisho ya Miaka 60 ya Chuo hicho yaliofanyika UDSM tarehe 29/01/2022. Mkuu wa WWilaya ya Ubungo Mhe.Kheri James akizungumza katika Shindano la Muziki la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwenye Maadhimisho ya Miaka 60 ya Chuo hicho yaliofanyika UDSM tarehe 29/01/2022. Mmoja wa wasanii wa nyimbo za kinyaturu mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam akitumbuiza katika Shindano la Muziki la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwenye Maadhimisho ya Miaka 60 ya Chuo hicho yaliofanyika UDSM tarehe 29/01/2022.Mmoja wa wasanii wa nyimbo za kisukuma mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam akitumbuiza katika Shindano la Muziki la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwenye Maadhimisho ya Miaka 60 ya Chuo hicho yaliofanyika UDSM tarehe 29/01/2022.Mmoja wa wasanii wa nyimbo za kimakonde mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam akitumbuiza katika Shindano la Muziki la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwenye Maadhimisho ya Miaka 60 ya Chuo hicho yaliofanyika UDSM tarehe 29/01/2022. Kwaya Kuu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakitumbuiza katika katika Shindano la Muziki la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwenye Maadhimisho ya Miaka 60 ya Chuo hicho yaliofanyika UDSM tarehe 29/01/2022. Wanamuziki Farid Kubanda (Fid Q) pamoja na Hamis Mwijuma (Mwana FA) wakifuatilia Shindano la Muziki la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwenye Maadhimisho ya Miaka 60 ya Chuo hicho yaliofanyika UDSM tarehe 29/01/2022. Baadhi ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakifuatilia Shindano la Muziki la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwenye Maadhimisho ya Miaka 60 ya Chuo hicho yaliofanyika UDSM tarehe 29/01/2022. NAIBU Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa,Tamaduni na Michezo Mhe.Said Yakubu (katikati) akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe.Kheri James( wa pili kushoto), Makamu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Prof.William Anangisye (wa pili kutoka kulia) na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo cha Dar es salaam-UTAFITI Prof.Benadeta Killian wakiimba wimbo wa Taifa katika Tamasha la Muziki la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha dar es Salaam kwenye Maadhimisho ya Miaka 60 ya Chuo hicho.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

****************************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

NAIBU Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa,Tamaduni na Michezo Mhe.Said Yakubu amekabidhi zawadi ya washindi wa Mashindano ya Kuimba Chuo kwa Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika maadhimisho ya Miaka 60 ya Chuo hicho.

Akizungumza katika hafla hiyo Mhe.Yakubu ameupongeza uongozi wa Chuo hicho kuendeleza na kukuza vipaji vya muziki kwa vijana wa Chuo hicho kwa kuwapatia fursa kuoneshesha vipaji vyao na kuvikuza.

Amesema matamasha kama haya matumaini yake yawe endelevu ili kuendelea kuibua fursa kwa vijana kupitia sanaa ya muziki kwani sanaa ni ajira kwasasa.

"Kukuza matamasha kama haya ili kuibua vipaji kwa vijana na pia kuwa sehemu ya kuwa daraja kwa watu ambao wanahitaji kuonesha na kuvikuza vipaji vyao". Amesema Mhe.Yakubu.

Kwa Upande wake Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM),Prof.William Anangisye amesema Chuo kiliandaa Tamasha la Muziki la Wanafunzi ambao hushindana na kuibua vipaji

Amesema Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimekuwa kikitoa mchango mkubwa katika taifa kwakuwa ni kitovu cha Utafiti, ufundishaji na ujifunzaji.

"Wahitimu wengi wameajiriwa Serikalini, katika Sekta binfasi na mashirika ya Kimataifa kutokana na ubora wa wahitimu katika kufikiri, kuchanganua mambo na kutatua changamoto mbalimbali katika vituo vya kazi, jamii na taifa kwa ujumla". Amesema.

Mshindi wa kwanza wa Tamasha hilo amekabidhiwa kitita cha Shilingi Milioni moja za Kitanzania, Mshindi wa Pili akikabidhiwa shilingi Laki saba na mshindi wa Tatu akiondoka na kitita cha Shilingi laki tano.

Mshindi wa kwanza ambaye aliondoka na kitita hicho Moses Selestin, mshindi wa pili ni Rodhey Rutashwotwa na mshindi wa tatu ulienda kwa Calum Aloyce.

Post a Comment

0 Comments