Ticker

6/recent/ticker-posts

WAZIRI MULAMULA AZINDUA BARAZA LA UONGOZI LA CHUO CHA DIPLOMASIA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akizungumza kuzindua Baraza la Uongozi la Chuo cha Diplomasia (CFR) cha jijini Dar es Salaam katika hafla iliyofanyika chuoni hapo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Diplomasia (CFR) wakimsikiliza Waziri Mulamula wakati wa hafla ya uzinduzi wa Baraza hilo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Diplomasia (CFR) wakimsikiliza Waziri Mulamula wakati wa hafla ya uzinduzi wa Baraza hilo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Baraza la Chuo cha CFR Balozi Ramadhani Muombwa Mwinyi akizungumza neno la shukurani kwa Mhe. Waziri Mulamula baada ya uzinduzi wa Baraza la Chuo hicho uliofanyika jijini Dar es Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mulamula akimkabidhi kitendea kazi Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo cha CFR Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi katika hafla ya uzinduzi wa Baraza hilo iliyofanyika chuoni hapo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Diplomasia (CFR) baada ya kuzindua baraza hilo jijini Dar es Salaam.

***********************


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) amezindua Baraza la Uongozi la Chuo cha Diplomasia (CFR) na kuwataka wajumbe wa Baraza hilo kufanya mabadiliko katika uendeshji wa Chuo hicho huku wakizangatia muktadha wa uanzishwaji wake

Balozi Mulamula amewataka wajumbe wa baraza hilo kuwasiliana na mamlaka husika ili CFR ibaki katika muundo wake wa asili yakiwemo maudhui ya kuanzishwa kwa chuo hicho ili kutojitenga kabisa na kuktadha huo huku kikiangalia namna bora ya kujiendesha.

“leo hii tuko hapa kuzindua Baraza la Chuo, Mwenyekiti na wajumbe wa Baraza hili, naomba muwasiliane na Mamlaka husika ili kuona namna Chuo kitakavyoweza kuendelea kufuata na kutekeleza nia na madhumuni ya kuanzishwa kwake na huku mkiangalia namna ya kujiendesha,”alisema Balozi Mulamula.

Amesema pamoja na kuwa Chuo kinaangalia namna mbalimbali za kujiendesha lakini hakiondoi jukumu lake la asili ambalo lililenga kuanzishwa kwake.

Amelitaka Baraza hilo kuangalia upya na kuandaa kozi mbalimbali ambazo walikuwa wakipatiwa maafisa mambo ya nje ili kuwawezesha maafisa hao kwenda na wakati na kuongeza ujuzi.

Akizungumza katia uzinduzi huo Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine amesema Uteuzi wa wajumbe wa Baraza hilo la Chuo utasaidia Chuo katika utekelezaji wa majukumu yake hasa ikizingatiwa sifa za wajumbe wa baraza hilo.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho Balozi Ramadhani Muombwa Mwinyi amemuhakikishia Mhe. Waziri utayari wa wajumbe wa baraza hilo katika kutekeleza majukumu yake ili kukifanya chuo hicho kutimiza malengo yake.

Post a Comment

0 Comments