Ticker

6/recent/ticker-posts

RITA YAWAKARIBISHA WANANCHI NANENANE MBEYA


**********************

Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) umewakaribisha wananchi wote kutembelea katika banda lao ili kupata huduma kwenye maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Wakulima yanayofanyika mkoani Mbeya katika viwanja vya John Mwakangale almaarufu kama viwanja vya nanenane.

Huduma zinazopatikana katika banda la RITA ni, Usajili wa vyeti vya kuzaliwa kwa watu wote waliozaliwa Tanzania bara, elimu kwa umma kuhusu usajili wa Ndoa na Talaka, Ufilisi na Udhamini pamoja na huduma ya msaada wa kisheria kuhusu masuala ya Wosia na Mirathi.

Akiongea kutoka viwanjani hapo, Afisa Usajili Msaidizi Bi. Noela G. Ituga anasema kuwa "tunapenda kuwakaribisha sana wananchi wote wafike katika banda letu ili kufaidika na huduma zetu kwa urahisi kabisa ambapo pia tunasajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa hapahapa viwanjani kwa kila mtu aliyezaliwa ndani ya mipaka ya Tanzania bara hivyo basi wakulima na watanzania wote wasiokuwa na vyeti hivi muhimu watembelee katika banda la RITA kupata huduma zetu".

Maonesho hayo yaliyoanza tarehe mosi mwezi wa nane yanatarajiwa kufikia kilele tarehe nane ambapo kitaifa yanafanyika katika viwanja vya John Mwakangale almaarufu viwanja vya nanenane mkoani Mbeya na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa mheshimiwa Rais Samia Suluhu.


Post a Comment

0 Comments