Ticker

6/recent/ticker-posts

WANANCHI WAENDELEA KUTEMBELEA BANDA LA TBS NANE NANE JIJINI ARUSHA

Afisa Usalama wa Chakula (TBS), Bw.Edward Mwamilawa akimsaidia mteja kuingia kwenye mfumo kwa ajili ya kupata huduma ya kitaalum ya kusafirisha bidhaa nje ya nchi. Kaimu Meneja wa Kanda ya Kaskazini ( TBS) Bw. Deogratius Ngatunga akimuelimisha mdau kuhusu masuala ya viwango katika maonesho ya 28 ya 88 mkoani Arusha.

*********************

TBS imeshiriki maonesho ya 28 ya 88 jijini Arusha yanayofanyika katika viwanja vya 88 Njiro.Kauli mbiu Agenda 10/30:Kilimo ni Biashara, Shiriki kuhesabiwa kwa mipango bora ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Maonesho hayo yameanza rasmi tar 01/08/2022 na kufunguliwa rasmi tarehe 03/08/2022 na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw. John Mongela.

TBS ni wadau wakubwa ukizingatia lengo moja wapo ni kuwezesha biashara.

Tumewatembelea wajasiriamali kujua changamoto zao sambamba na kuwapa elimu ya kuthibitisha ubora wa bidhaa zao haswa ukizingatia kwa sasa kwao ni bure, Serikali inatenga kati ya 150M -200M kila mwaka kwa ajili ya kuwahudumia. Mpaka sasa zaidi ya wajadiriamali wadogo 600 kutoka mikoa mbalimbali wamepata leseni chini ya mpango huu wa bure.( Bw Deogratius Ngatunga, Kaimu Meneja wa TBS Kanda ya Kaskazini)

Meneja alisema TBS ipo viwanjani hapo pia kwa ajili ya kuwapa msaada wateja wapya na wazamani kwa kuwaelekeza jinsi ya kufanya maombi ya usajili wa bidhaa na majengo ya chakula na vipodozi pamoja na maombi ya kupata leseni ya kutumia alama ya ubora. 

Bw. Ngatunga alitoa wito kwa wateja na wananchi kutumia fursa hiyo kwa kutembelea banda la TBS lililopo ndani ya viwanja hivyo na watakaoshindwa wasisite kuwasiliana na TBS kupitia kituo cha huduma kwa wateja kwa namba ya bure 0800110827.

Maonesho haya yanatarajia kufungwa tarehe 08/08/2022 .

Post a Comment

0 Comments