Ticker

6/recent/ticker-posts

DKT.JAFO AFANYA ZIARA KUTEMBELEA MTO MSIMBAZI KATA YA MOGO MTAA WA KIPAWA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mheshimiwa Dkt. Selemani Jafo akiwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe.Ng`wilabuzu Ludigija wakiwa katika Mto Msimbazi kata ya Mogo mtaa wa Kipawa Jijini Dar es Salaam mara baada ya kutembelea eneo hilo leo Oktoba 18,2022.Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mheshimiwa Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Mwenyekiti wa Kikosi kazi cha kuratibu usafishaji wa Mito na mabonde Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Elizabeth Mshote mara baada ya kufanya ziara ya kutembelea Mto Msimbazi kata ya Mogo mtaa wa Kipawa leo Oktoba 18,2022 Jijini Dar es Salaam Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mheshimiwa Dkt. Selemani Jafo akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufanya ziara ya kutembelea Mto Msimbazi kata ya Mogo mtaa wa Kipawa leo Oktoba 18,2022 Jijini Dar es Salaam Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mheshimiwa Dkt. Selemani Jafo akipata picha ya pamoja na wakazi wa Mto Msimbazi kata ya Mogo mtaa wa Kipawa Jijini Dar es Salaam mara baada ya kutembelea eneo hilo leo Oktoba 18,2022. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mheshimiwa Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza mmoja wa mkazi wa eneo la Mogo mtaa wa Kipawa mara baada ya kutembelea Mto Msimbazi uliopita eneo hilo leo Oktoba 18,2022 Jijini Dar es Salaam Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mheshimiwa Dkt. Selemani Jafo akielekeza jambo akiwa katika Mto Msimbazi kata ya Mogo mtaa wa Kipawa Jijini Dar es Salaam mara baada ya kutembelea eneo hilo leo Oktoba 18,2022.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mheshimiwa Dkt. Selemani Jafo akiwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe.Ng`wilabuzu Ludigija wakiwa katika Mto Msimbazi kata ya Mogo mtaa wa Kipawa Jijini Dar es Salaam mara baada ya kutembelea eneo hilo leo Oktoba 18,2022.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mheshimiwa Dkt. Selemani Jafo akiwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe.Ng`wilabuzu Ludigija wakiwa katika Mto Msimbazi kata ya Mogo mtaa wa Kipawa Jijini Dar es Salaam mara baada ya kutembelea eneo hilo leo Oktoba 18,2022. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira Mheshimiwa Dkt. Selemani Jafo akiwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe.Ng`wilabuzu Ludigija wakimsikiliza mmoja wa wasimamizi wa shughuli katika Mto Msimbazi kata ya Mogo mtaa wa Kipawa Jijini Dar es Salaam mara baada ya kutembelea eneo hilo leo Oktoba 18,2022.

***************************

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mheshimiwa Dkt. Selemani Jafo ametoa muda wa siku nne kwa Kikosi kazi cha kusimamia Muongozo wa usafishaji mchanga kwa Mkoa wa Dar es Salaam kumpelekea taarifa ya nini kifanyike kuhusiana na kutafuta suluhisho na kupata ufumbuzi juu ya athari zinazotokana na uchimbaji wa mchanga katika Mto Msimbazi.

Ameyasema hayo leo Oktoba 17,2022 Jijini Dar es Salaam alipokua katika ziara ya kutembelea Mto Msimbazi katika Kata ya Mogo Mtaa wa Kipawa katika jiji la Ilala Mkoani Dar es Salaam.

“Nimekuja hapa sababu Ofisi yangu imepokea malalamiko kuhusiana na athari za kimazingira zinazotokana na suala zima la usafishaji wa mto huu wa Msimbazi. Na kwa sababu kuna mawazo kinzani kutoka kwa pande mbili. Ninawapa siku tano mjadiliane kwa kina nini kifanyike na mniletee taarifa hiyo Ofisini kwangu”.

Aidha ameongeza kuwa baada ya kufika katika eneo hilo la Mto huo amesikiliza maoni ya Wananchi na amepata maoni yanayokinzana kwani wengine wanasema baada ya shughuli za usafishaji mto huo kuanza zimeleta athari kwa mazingira na wengine wamesema baada ya shughuli hizo kuanza usafishaji umeleta manufaa makubwa kwa jamii inayozunguka eneo hilo.

Akiongea baada ya maelekezo hayo Mkuu wa Wilaya wa Manispaa ya Ilala Mheshimiwa Ng’wilabuzu Ludigija amemuhakikishia Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mheshimiwa Dkt. Selemani Jafo kuwa amepokea maelekezo hayo na watayafanyia kazi na kuyasimamia kwa karibu sana.

Naye Meneja wa NEMC Kanda ya Mashariki- Kaskazini Bw. Arnold Mapinduzi amesema kuwa Muongozo wa usafishaji mchanga umeelekeza suala hilo lifanyike kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa ikiwa ni pamoja wote wanaotaka kujishughulisha na suala hilo waombe vibali kutoka Mamlaka yay a Usimamizi wa Bonde la Wami Ruvu.

Post a Comment

0 Comments