Ticker

6/recent/ticker-posts

WIZARA YA ELIMU YANG'ARA RIADHA KATIKA MICHUANO YA SHIMIWI



Na Oscar Assenga,TANGA

TIMU ya Mchezo wa Riadhaa ya Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia imeng’ara katika Mashindano ya Shimiwi yanayoendelea Jijini Tanga.

Wachezaji wa timu ya Elimu ilianza kwa kasi katika mchezo huo wa Riadhaa ambapo wakimbiaji wake walikuwa hari kubwa ya kukimbiza upepo ili kuweza kupata ushindi katika mashindano hayo.

Katika mchezo huo timu ya wanaume imefanya vizuri kwa upande wa mita 100 kupokezana vijiti huku kwenye zile za mita 200 wakiibuka washindi wa pili.

Kwa upande wa michezo mengine timu za Wizara hiyo walipambana mpaka kufikia hatua ya nane bora kwa mchezo wa kuvuta kamba ,mpira wa miguu,mpira wa pete .

Akizungumza kuhusu mashindano hayo Makamu Mwenyekiti ywa timu ya Elimu Sports Deogratius Wenga alisema kwamba mashindano hayo yamekuwa na ushindani mkubwa.



Post a Comment

0 Comments