Ticker

6/recent/ticker-posts

KIJANA ALIYEOKOA ABIRIA NDEGE IKIWA ZIWANI APEWA KAZI JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI

Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV

Kijana aliyefahamika kwa jina la Majaliwa Jackson ambaye anafanya shughuli za Uvuvi katika Ziwa Victoria amependekezwa kuingizwa kwenye Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ili kupata mafunzo zaidi katika Jeshi hilo baada ya kuonyesha ujasiri mkubwa katika zoezi la uokoaji wa Manusura wa ajali ya Ndege ya Precision Air iliyotokea Novemba 6, 2022 katika Ziwa Victoria mkoani Kagera.


Agizo hilo limetolewa na Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ambaye yupo ziarani nje ya nchi, kupitia kwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye alitoa hotuba katika zoezi la kuaga miili ya watu 19 waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo.


“Kwa ujasiri alionyesha Kijana huyu, Mhe Rais ameagiza Kijana huyu akabidhiwe kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ili apate mafunzo ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ili kupata mafunzo zaidi ya Uokoaji”, amesema Kassim Majaliwa.


Aidha, Waziri Mkuu ameagiza Serikali kuhakikisha Wavuvi waliopo kwenye eneo hilo la Ziwa Victoria wanapatiwa mafunzo ya Uokoaji.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema Serikali itagharamia mazishi ya watu wote waliofariki kwenye ajali hiyo.

Post a Comment

0 Comments