Ticker

6/recent/ticker-posts

BARRICK YADHAMINI NA KUSHIRIKI KONGAMANO LA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU NCHINI - AIESEC

Afisa Raslimali Watu wa Barrick Bulyanhulu, Alpha Gonzi,akiongea na wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali wakati wa kongamano la AIESEC lililofanyika ukumbi wa Nkurumah katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa udhamini wa kampuni ya Barrick.
Baadhi ya wanafunzi waliohudhuria kongamano hilo wakipata ufafanuzi wa shughuli za kampuni ya Barrick kutoka kwa maofisa wa kampuni hiyo.
Wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali wakifuatilia mada za kuwajengea uwezo wa kukabili ushindani na kuhimili kufanya kazi kwa ufanisi watakapomaliza masomo yao zilizotolewa na Maofisa waandamizi kutoka makampuni mbalimbali nchini wakati wa kongamano hilo.
Wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali wakifuatilia mada za kuwajengea uwezo wa kukabili ushindani na kuhimili kufanya kazi kwa ufanisi watakapomaliza masomo yao zilizotolewa na Maofisa waandamizi kutoka makampuni mbalimbali nchini wakati wa kongamano hilo.
Wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali wakifuatilia mada za kuwajengea uwezo wa kukabili ushindani na kuhimili kufanya kazi kwa ufanisi watakapomaliza masomo yao zilizotolewa na Maofisa waandamizi kutoka makampuni mbalimbali nchini wakati wa kongamano hilo.
Wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali wakifuatilia mada za kuwajengea uwezo wa kukabili ushindani na kuhimili kufanya kazi kwa ufanisi watakapomaliza masomo yao zilizotolewa na Maofisa waandamizi kutoka makampuni mbalimbali nchini wakati wa kongamano hilo.
Baadhi ya wanafunzi walipata fursa ya kupiga picha ya pamoja na wawakilishi wa makampuni yaliyoshiriki kwenye kongamano hilo na viongozi wa taasisi ya AIESEC
***

Kampuni ya Barrick, imeeleza dhamira yake ya kuendelea kuibua na kukuza vipaji vya vijana wasomi wa vyuo vya elimu ya juu na kati nchini ili waweze kukabiliana na mabadiliko yanayoendelea kutokea duniani na kuhimili ushindani katika soko la ajira sambamba na kuweza kujiamini kutumia ujuzi na taaluma zao kujiajiri kwa ajili ya kujenga mustakabali endelevu.


Hayo yameeleza na Afisa Mwandamizi wa Raslimali Watu wa Barrick Bulyanhulu Alpha Gonzi, wakati wa kongamano la wanafunzi wa vyuo vikuu lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) lililoandaliwa na taasisi ya kuchipua na kuendeleza vipaji vya uongozi kwa vijana (AIESEC na kudhaminiwa na kampuni ya Barrick.

Post a Comment

0 Comments