Ticker

6/recent/ticker-posts

CHUO CHA TAIFA CHA UTALII (NCT) CHAHITIMISHA MAFUNZO YA UANAGENZI JIJINI DAR



Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) Jesca William, Akizungumza katika hafla ya kukabidhi vyeti kwa wanafunzi wa Kozi fupi ya Uanagenzi iliyofanyika Mei 24,2023 Jijini Dar es Salaam DAR ES SALAAM. 

Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) kimehitimisha rasmi mafunzo ya muda mfupi ya Uanagenzi yaliyodhaminiwa na Shirika la giZ kupitia mradi wa E4D. 

Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) yamelenga kutoa ujuzi kwa vijana katika fani mbalimbali yatakayo wawezesha kuingia katika soko la ajira kwenye Sekta ya Utalii na kujiajiri wenyewe. 

Akizungumza katika hafla hiyo kwa niaba ya Makamu Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) Dkt. Florian Mtey, Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo hicho Jesca William, amesema mafunzo hayo yamelenga kuongeza msukumo katika kuchangamkia fursa za ajira katika sekta hiyo kwa kuzingatia kwamba Sekta ya Utalii inazidi kukua, na watalii kuongezeka kutokana na filamu maarufu ya 'The Royal Tour' iliyozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. 

Kwa upande wake Afisa utumishi Halmashahuri ya Jiji la Dar es Salaam William Matto, akizungumza katika hafla hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji hilo, amesema Serikali imeendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wadau wa maendeleo katika kuhakikisha wanawafikia vijana wengi zaidi. 

Aidha amewataka wahitimu hao kutumia vyema mafunzo waliyoyapata Chuoni hapo kwa kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa weledi. 

Nao baadhi ya wanufaika wa program hiyo wamesema kuwa, mafunzo hayo yamewasaidia kuongeza maarifa hasa katika kutekeleza majukumu yao pamoja na kuanzisha miradi binafsi. 

Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) kimefanikiwa kutoa wahitimu zaidi 400 tangu kuanzishwa kwa programu ya Uanagenzi Chuoni hapo, kuanzia mwaka 2014 hadi 2022 katika ngazi ya Stashahada. 

(PICHA ZOTE NA: HUGHES DUGILO) 

Afisa utumishi Halmashahuri ya Jiji la Dar es Salaam William Matto, akizungumza katika hafla hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji hilo. 

Meneja Miradi wa giZ Costantine Shirati, akizungumza katika hafla hiyo. 

Baadhi ya Wahitimu wakipokea vyeti.. 

Baadhi ya Wakufunzi wa NCT wakiwa na wanafunzi tayari kwa kukata keki maalum katika hafla hiyo. 

Mkufunzi kutoka Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) Mary Maduhu akizungumza alipokuwa akitoa neno la shukrani kwenye hafla hiyo. 


Picha za pamoja.

Post a Comment

0 Comments