Ticker

6/recent/ticker-posts

JIOPAKI PEKEE KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA KUANZISHWA NGORONGORO -MCHENGERWA


Na John Mapepele

Waziri wa Maliasili na Utalii - Mhe. Mohammed Mchengerwa amepokea timu ya wataalam saba kutoka nchini China ambao wamewasili nchini kwa ajili ya kuanza maandalizi ya utekelezaji wa mradi wa uendelezaji wa jiopaki ya Ngorongoro- Lengai, ambayo ndio jipaki pekee kusini kwa Jangwa la Sahara .

Pamoja na uimarishaji wa uhifadhi wa rasilimali za kijiolojia, mradi huu utaongeza vivutio vya utalii, ujenzi wa makumbusho ya kijiolojia, kuweka mitambo ya kufuatilia hatari za kijiolojia na kuwajengea uwezo wataalam wa kitanzania kuwezesha ukuaji utalii wa miamba na sura za nchi ( Geotourism and landscape tourism)

Mradi huu ambao utagharimu jumla ya dolla za kimarekani millioni 9.5 na kutarajiwa kukamilika baada ya miaka miwili na nusu, umefadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China.

Makubaliano ya msaada huu yalisainiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alipofanya ziara ya kitaifa nchini China Novemba, 2022.
Mhe. Mchengerwa amefafanua kuwa dhamira ya Serikali kwa sasa ni kuimarisha uhifadhi wa raslimali na kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii kimataifa na kutoa wito kwa wananchi kushirikiana kikamili kwa faida ya kizazi cha sasa na baadaye.

Post a Comment

0 Comments