Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS DKT.MWINYI AWAAHIDI WAZANZIBAR KUWAPUNGUZIA UMASIKINI

04 Novemba, 2023

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amewaahidi Wanzanzibari kuwapunguzia umasikini kabla ya mwaka 2025 kwa kuwaongezea miradi mikubwa ya maendeleo.

Amesema, amekusudia kuikamilisha kwa vitendo Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025 kwa miaka miwili iliyobakia ya uongozi wake na kuikamilisha miradi mkikubwa ya kimkakati ya Bandari Jumuishi ya Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini Unguja, barabara za kutulia na kurukia ndege pamoja na jengo kubwa la abiria katika uwanja wa ndege wa Pemba vinavyotarajiwa kugharimu zaidi ya dola za Marekeni milioni 400.

Dk. Mwinyi ambae ni Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, CCM- Zanzibar aliyasema hayo, viwanja vya Maisara Suleiman Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi, alipozungumza na Wazanzibari kwenye maadhimisho ya miaka mitatu ya uongozi wake, tokea alipoingia madarakani kuiongoza awamu ya nane ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, mwezi Novemba mwaka 2020.

Pia, Rais Dk. Mwinyi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan kwa mchango mkubwa alioutoa kwa maendeleo ya Zanzibar na kuongeza kuwa hatua ya maendeleo iliyofikiwa ndani ya visiwa vya Unguja na Pemba kuna mkono wa Rais Dk. Samia.

Akizungumzia suala la amani, umoja na mshikamano, Rais Dk. Mwinyi alisema maendeleo makubwa yaliyofikiwa Zanzibar ndani ya kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wake, yametona na juhudi kubwa ya wananchi wa Zanzibar, kuendelea kuidumisha amani iliopo, umoja na mshikamano wao, umetoa fusra nzuri ya kutendeka mafanikio yote hayo.

Aidha, Rais Dk. Mwinyi aliahidi kuongeza tena kasi ya maendeleo kwa kipindi cha miaka miwili iliyobakia. Pia aliwapongeza Umoja wa Wanawake Tanzania, (UWT) kwa kazi kubwa wanayoifanya nchi nzima, kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM na miradi ya Maendeleo Tanzania bara na visiwani.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Mwenyeketi wa UWT Taifa, Merry Chattanda alipongeza juhudi kubwa ya mafanikio iliyofikiwa na awamu ya nane ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwenye sekta zote za maendeleo ikiwemo ujenzi wa barabra, Skuli, hospitali 10 za wilaya na moja ya mkoa iliyokamilishwa kwa miundombinu na vifaa vya kisasa, ongezeko la ajira kwa vijana kupitia sekta za ujenzi wa miundombinu, utalii, ujasiriamali, biashara na kilimo cha umwagiliji wa mpunga, hali aliyoielezea matarajio ya Zanzibar kujiwekea akiba ya chakula.

Pia, Chattanda alimpongeza Rais. Dk. Mwinyi kwa kufanikiwa kuwakomboa wanawake wa Zanzibar dhidi ya changamoto cha maji safi na salama kwa kuwajengea visima vikubwa vya maji, Unguja na Pemba pamoja na kuwasambazia mabomba, kuwawekea usafiri wa haraka baharini kisiwani Pemba.

Aidha, Chattanda alisifu mchango mkubwa unaotolewa na Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation kupitia Mwenyekiti wake wa Bodi, Mama Mariam Mwinyi, Mke wa Rais wa Zanzibar kwa kuwezesha kinamama wengi wakulima wa mwani na kuwajengea kiwanda kikubwa cha kusarifu mwani, eneo la Chamanangwe, Pemba.

Mapema, akiwasilisha salamu za Chama cha Mapinduzi viwanjani hapo, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Bara, Abdul Rahman Kinana aliwasihi Wazanzibari kuendelea kuidumisha amani na mshikano uliopo baina yao na kuendelea kushirikiana na viongozi wao wa Serikali kuijenga Zanzibar.

Sherehe za maadhimisho ya miaka mitatu ya mafanikio ya awamu ya nane ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, zilliandaliwa na kufanikishwa na Jumuiya ya CCM ya Umoja wa Wanawake, Tanzania (UWT)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambae pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhiwa zawadi maalum iliyotolewa na UWT Taifa ya kumpongeza kwa Uongozi wake wa Miaka Mitatu, akikabidhiwa na Mwenyekiti wa UWT Taifa Mhe. Mary Chatanda, wakati wa mkutano huo uliyofanyika katika viwanja vya Maisara Suleiman Wilaya ya Mjini Unguja leo 4-11-2023.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambae pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhiwa zawadi maalum iliyotolewa na UWT Taifa ya kumpongeza kwa Uongozi wake wa Miaka Mitatu, akikabidhiwa na Mwenyekiti wa UWT Taifa Mhe. Mary Chatanda, wakati wa mkutano huo uliyofanyika katika viwanja vya Maisara Suleiman Wilaya ya Mjini Unguja leo 4-11-2023.(Picha na Ikulu)


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na kumpongeza Msanii wa muziki wa Kizazi Kipya Tanzania Zuchu baada ya kumaliza kutowa burudani, wakati wa Mkutano Maalum wa Kumpongeza kwa Uongozi wake wa Miaka Mitatu ulioandaliwa na Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT) Taifa katika viwanja vya Maisara Suleiman Wilaya ya Mjini Unguja leo 4-11-2023.(Picha na Ikulu)
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM Tanzania Mhe.Merry Chatanda akisalimia Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini Kichama Ndg.Talib Ali Talib pamoja na Viongozi wengine alipowasili viwanja vya Maisara Suleiman Jijini Zanzibar katika shere maalum iliyoandaliwa leo na Jumuiya hiyo kwa jaili ya kumpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi kwa kutimiza miaka mitatu ya Uongozi wake. [Picha na Ikulu]04/11/2023.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi na Mkewe Mama Mariam Mwinyi alipokuwa akisalimiana na Viongozi wakati alipowasili viwanja vya Maisara Suleiman Jijini Zanzibar leo katika hafla maalum ya kupongezwa na Umoja wa Wanawake wa CCM Tanzania kwa kutimiza miaka mitatu ya Uongozi wake.[Picha na Ikulu]04/11/2023.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi (katikati) pamoja na Viongozi wengine wakisimama wakati Wimbo wa Taifa ukipigwa katika sherehe maalum za kupoongewa kwa Kutimiza miaka mitatu ya Uongozi wake,zilizofanyika leo katika viwanja vya Maisara Suleiman Jijini Zanzibar kwa kuandaliwa na Jumuiya ya Wanawake wa CCM Tanzania Chi na Uongozi wa Mwenyekiti wake Mhe.Merry Chatanda(wa tatu kushoto).[Picha na Ikulu] 04/11/2023.

Makamo Mwenyekiti wa CCM Bara Mhe.Abdulrahmani Kinana (kulia) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi (katikati) na Mke wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Sala Kikwete wakiwa katika sherehe maalum za kupoongewa kwa Kutimiza miaka mitatu ya Uongozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi,zilizofanyika leo katika viwanja vya Maisara Suleiman Jijini Zanzibar ambazo zimeandaliwa na Jumuiya ya Wanawake wa CCM Tanzania . [Picha na Ikulu] 04/11/2023.
Vikundi mbali mbali vya Wasanii Vikitoa burudani wakati wa sherehe za kupongezwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi,zilizofanyika leo katika viwanja vya Maisara Suleiman Jijini Zanzibar ambazo zimeandaliwa na Jumuiya ya Wanawake wa CCM Tanzania kwa kutimiza miaka mitatu ya Uongozi wake . [Picha na Ikulu] 04/11/2023.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi (kushoto) akikabidhi mfanno wa Cheki ya Fedha tasilimu Millioni Sabiini na Tano ,zilizotolewa Benki ya CRDB kwa ajili ya uwezeshaji wa Vikundi 17 vya Wanawake Zanzibar katika sherehe maalum za kupoongewa kwa Kutimiza miaka mitatu ya Uongozi wake,zilizofanyika leo katika viwanja vya Maisara Suleiman Jijini Zanzibar kwa kuandaliwa na Jumuiya ya Wanawake wa CCM Tanzania. [Picha na Ikulu] 04/11/2023.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi alipokuwa akitoa hutuba yake katika mkutano maalum wa kupongezwa kwa kutimiza miaka mitatu ya Uongozi wake leo katika viwanja vya Maisara Suleiman Jijini Zanzibar kwa kuandaliwa na Jumuiya ya Wanawake wa CCM Tanzania. [Picha na Ikulu] 04/11/2023.Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi alipokuwa akiwapungia mkono Wanachama na Viongozi wa CCM wakati akiondoka katika mkutano maalum wa kupongezwa kwa kutimiza miaka mitatu ya Uongozi wake leo katika viwanja vya Maisara Suleiman Jijini Zanzibar, ulioandaliwa na Jumuiya ya Wanawake wa CCM Tanzania. [Picha na Ikulu] 04/11/2023.

Post a Comment

0 Comments