Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Thomas Lutachunzibwa (aliyesimama kulia), akifunga mafunzo ya kudhibiti matukio ya sumu kwa wataalamu wa Afya yaliyofanyika katika ukumbi wa Profesa Manyele jijini Dodoma- Septemba 13,2024.
Mkuu wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu, Yohana Goshashy (aliyesimama, picha ya kwanza),akiwasilisha mada kwa wataalamu wa Afya kuhusu majukumu yanayotolewa na Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu katika mafunzo ya kudhibiti matukio ya sumu kwa wataalamu hao yaliyofanyika katika ukumbi wa Profesa Manyele uliopo Makao makuu ya Mamlaka, jijini Dodoma, Septemba 13,2024.
Meneja wa Maabara ya Sayansi Jinai Toksikolojia, Kagera Ng’weshemi (aliyesimama kulia), akiwasilisha mada kuhusu majukumu yanayotekelezwa na Maabara ya Toksikolojia katika mafunzo ya kudhibiti matukio ya sumu kwa wataalamu wa Afya yaliyofanyika katika ukumbi wa Profesa Manyele jijini Dodoma, Septemba 13,2024.
Mtumishi wa Mamlaka, Christer Mwageni (aliyesimama), akieleza hali ya matukio ya sumu nchini na kwa Mkoa wa Dodoma kwa kipindi cha miaka mitano katika mafunzo ya kudhibiti matukio ya sumu kwa wataalamu wa Afya yaliyofanyika katika ukumbi wa Profesa Manyele uliopo jijini Dodoma, Septemba 13,2024.
Wataalamu wa Afya wakifuatilia mada mbalimbali zilizowasilishwa na watumishi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali katika mafunzo ya kudhibiti matukio ya sumu kwa wataalamu wa Afya yaliyofanyika katika ukumbi wa Profesa Manyele jijini Dodoma, Septemba 13,2024.
0 Comments