Ticker

6/recent/ticker-posts

MBUNGE RWAKATARE AWATEMBELEA MABINTI 300 FDC IFAKARA, AWAPATIA MAHITAJI MUHIMU

Mhe Mbunge wa Jimbo la Mlimba,Dkt KellenRose Rwakatare, ametembelea mabinti 300 wanaosoma katika Chuo cha Maendeleo FDC Ifakara na kuwapatia mahitaji mbalimbali muhimu kwa ajili ya kuendeleza masomo yao ya ufundi stadi.

Ziara hiyo imelenga kuwatia moyo, kuwasikiliza pamoja na kuthibitisha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika kuwawezesha vijana wa kike kielimu na kiuchumi.

Akizungumza na mabinti hao, Mhe Mbunge aliwahimiza kusoma kwa bidii, kutumia vyema fursa waliyoipata na kuwa chachu ya mabadiliko katika jamii. Ziara hiyo pia ilisindikizwa na viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Kilombero waliopongeza juhudi hizo za maendeleo

Post a Comment

0 Comments